-
“Uendako Nitaenda”Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 1
-
-
Huku akimtazama Naomi wakiwa kwenye barabara hiyo isiyo na watu, Ruthu alikuwa na uhakika na utulivu moyoni. Moyo wake ulikuwa na upendo mwingi kumwelekea Naomi, na Mungu ambaye Naomi aliabudu. Hivyo akasema: “Usiniombe nikuache, nigeuke nisifuatane nawe; kwa maana uendako nitaenda, na mahali utakapokaa usiku kucha nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako Mungu wangu. Pale utakapokufa nitakufa nami, na hapo ndipo nitakapozikwa. Yehova na anitende hivyo na kuzidi ikiwa chochote isipokuwa kifo kitatutenganisha mimi na wewe.”—Ruthu 1:16, 17.
Maneno ya Ruthu yalikuwa ya pekee sana, hivi kwamba bado yanakumbukwa hata baada ya miaka elfu tatu kupita. Maneno yake yanafafanua vizuri sifa yenye thamani, yaani, upendo mshikamanifu. Ruthu alikuwa na upendo wenye nguvu na wenye ushikamanifu sana hivi kwamba alikuwa tayari kushikamana na Naomi na kwenda popote pale pamoja naye. Wangetenganishwa tu na kifo. Watu wa Naomi wangekuwa watu wake, kwa kuwa Ruthu alikuwa tayari kuacha kila kitu alichokijua huko Moabu, hata miungu ya Wamoabu. Tofauti na Orpa, Ruthu alisema kwa moyo wote kwamba alitaka Mungu wa Naomi, Yehova, awe Mungu wake pia.b
-
-
“Uendako Nitaenda”Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 1
-
-
b Inapendeza kuona kwamba Ruthu hakutumia tu jina la cheo “Mungu” kama vile ambavyo watu wengi wa mataifa ya kigeni wangefanya; alitumia pia jina la kibinafsi la Mungu, Yehova. Tafsiri ya The Interpreter’s Bible inasema hivi: “Hivyo basi, mwandikaji anakazia kwamba mgeni huyo ni mfuasi wa Mungu wa kweli”
-