-
Mafundisho Kuhusu Kukosa UaminifuUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
6. (a) Ni hali gani zaenea ndani ya Yerusalemu? (b) Kwa nini wengine wafurahi, lakini kuna nini mbele?
6 Isaya aendelea: “Ewe uliyejaa makelele, mji wa ghasia, mji wenye furaha; watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.” (Isaya 22:2) Umati wa watu umeingia jijini, nalo limejaa makelele. Watu mitaani wanapiga makelele nao wanahofu. Hata hivyo, baadhi yao wanafurahi, labda kwa sababu wanahisi wako salama au wanaamini kuwa hatari inapitilia mbali.a Lakini ni upumbavu kufurahi wakati huu. Wengi jijini humo watakufa kifo chenye ukatili zaidi kuliko kile cha upanga. Jiji lililozingiwa halina njia yoyote ya kupata chakula kutoka nje. Akiba zilizo ndani ya jiji zapungua. Watu wanaokufa njaa na hali zenye kusongamana zasababisha magonjwa ya mlipuko. Kwa hiyo wengi jijini Yerusalemu watakufa kutokana na njaa na magonjwa ya kuambukiza. Mambo hayo yatukia mwaka wa 607 K.W.K. na vilevile mwaka wa 70 W.K.—2 Wafalme 25:3; Maombolezo 4:9, 10.b
-
-
Mafundisho Kuhusu Kukosa UaminifuUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Mwaka wa 66 W.K., Wayahudi wengi walifurahi majeshi ya Roma yaliyokuwa yakizingira Yerusalemu yalipoondoka.
-