-
Maneno Manne Yaliyoubadili UlimwenguSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
10. Watu wenye hekima walifanikiwa kiasi gani katika jitihada zao za kufasiri maandishi ya mkono ukutani?
10 Watu wenye hekima wakaingia katika jumba hilo kubwa. Walikuwa wengi kwa kuwa Babiloni lilikuwa jiji lililojaa dini zisizo za kweli na lenye mahekalu mengi. Bila shaka, kulikuwako watu wengi waliodai kuweza kubashiri mambo na kufumbua maandishi ya kifumbo. Lazima watu hao wenye hekima walisisimuka walipopata fursa hiyo. Sasa walikuwa na fursa ya kudhihirisha uwezo wao mbele ya waheshimiwa, mfalme apendezwe nao, na kupewa cheo kikubwa sana. Lakini walishindwa kama nini! “Hawakuweza kuyasoma yale maandiko, wala kumjulisha mfalme tafsiri yake.”d—Danieli 5:8.
11. Huenda ni kwa nini watu wenye hekima wa Babiloni walishindwa kuyasoma maandishi hayo?
11 Hatuna uhakika ikiwa watu wenye hekima wa Babiloni walishindwa kufumbua maandishi hayo yenyewe, yaani herufi zenyewe. Ikiwa ndivyo ilivyokuwa, wafidhuli hao wangekuwa na fursa ya kutosha ya kubuni fasiri yoyote ile ya udanganyifu, labda hata wakimsifusifu mfalme isivyo kweli. Yawezekana pia kwamba herufi hizo zingeweza kusomeka vizuri. Hata hivyo, kwa kuwa lugha kama vile Kiaramu na Kiebrania ziliandikwa bila vokali kila neno lingaliweza kuwa na maana kadhaa. Ikiwa ndivyo ilivyokuwa, huenda watu hao wenye hekima walishindwa kuamua ni maneno gani yaliyokusudiwa. Hata ikiwa wangejua ni maneno gani, bado hawangeweza kufahamu maana ya maneno hayo ili waweze kuyafasiri. Vyovyote vile, kwa hakika: Watu wenye hekima wa Babiloni walishindwa vibaya!
-
-
Maneno Manne Yaliyoubadili UlimwenguSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
d Jarida Biblical Archaeology Review lataarifu hivi: “Wataalamu Wababiloni waliandika maelfu ya ishara zenye kuashiria mabaya . . . Belshaza alipotaka kujua maana ya maandishi yaliyokuwa ukutani, yawezekana kwamba wenye hekima wa Babiloni walichunguza vitabu vya ishara hizo. Lakini havikuwasaidia.”
-