Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Tenda Haki’ Unapotembea na Mungu
    Mkaribie Yehova
    • 13 Tukielewa kwamba haki ya Mungu ni yenye rehema, hatutafanya haraka kuwahukumu wengine katika mambo ambayo hayatuhusu au mambo yasiyo na maana sana. Katika Mahubiri yake ya Mlimani, Yesu alionya hivi: “Komeni kuhukumu ili msipate kuhukumiwa.” (Mathayo 7:1) Kulingana na simulizi la Luka, Yesu aliongezea hivi: “Komeni kulaumu, nanyi hamtalaumiwa kwa vyovyote.”a (Luka 6:37) Yesu alitambua kwamba wanadamu wasiokamilika wana mwelekeo wa kuhukumu-hukumu. Msikilizaji yeyote aliyekuwapo mwenye tabia ya kuhukumu-hukumu wengine vikali alipaswa kukoma kufanya hivyo.

      14. Kwa nini tunapaswa ‘kukoma kuhukumu’ wengine?

      14 Kwa nini ni lazima ‘tukome kuhukumu’ wengine? Kwanza, mamlaka yetu ina mipaka. Mwanafunzi Yakobo atukumbusha hivi: “Mmoja yuko ambaye ni mpaji-sheria na hakimu,” yaani, Yehova. Kisha Yakobo anauliza hivi waziwazi: “Wewe ni nani uwe ukihukumu jirani yako?” (Yakobo 4:12; Waroma 14:1-4) Isitoshe, ni rahisi sana kuwahukumu wengine isivyo haki kwa sababu sisi ni wenye dhambi. Mitazamo na mielekeo mbalimbali—kama vile ubaguzi, kuudhika, wivu, na kujiona kuwa mwadilifu—inaweza kupotosha maoni yetu juu ya wanadamu wengine. Hatutafanya haraka kutafuta makosa ya wengine ikiwa tutakumbuka kwamba hata sisi tuna udhaifu. Hatuwezi kusoma mioyo; wala hatuwezi kujua kikamili hali za wengine. Basi, sisi ni nani hata tuwatilie shaka waamini wenzetu au kuchambua jitihada zao za kumtumikia Mungu? Itakuwa vyema tukimwiga Yehova kwa kukazia fikira mambo mazuri ambayo ndugu na dada zetu wanafanya badala ya kutafuta tu kasoro zao.

      15. Waabudu wa Yehova hawapaswi kamwe kutenda kwa njia gani na kutumia maneno ya aina gani, na kwa nini?

      15 Vipi kuhusu watu wa familia yetu? Inasikitisha kwamba leo hukumu kali zaidi hutolewa nyumbani, mahali ambapo panapaswa kuwa na amani. Ni kawaida kusikia kuhusu waume, wake, au wazazi wakatili ambao huwatukana daima au kuwajeruhi watu wa familia yao. Lakini waabudu wa Mungu hawapaswi kamwe kutumia maneno makali, kufanya mzaha wenye kuumiza, au kuwajeruhi wengine. (Waefeso 4:29, 31; 5:33; 6:4) Shauri la Yesu la ‘kukoma kuhukumu’ na ‘kukoma kulaumu’ linapasa kufuatwa nyumbani pia. Kumbuka kwamba kuonyesha haki kunatia ndani kuwatendea wengine jinsi Yehova anavyotutendea. Na Mungu wetu hatutendei kamwe kwa ukali au kwa ukatili. Badala yake, yeye “ni mwenye wororo sana katika shauku” kwa wale wanaompenda. (Yakobo 5:11) Yeye ni mfano bora sana wa kuiga!

  • ‘Tenda Haki’ Unapotembea na Mungu
    Mkaribie Yehova
    • a Tafsiri nyingine husema “usihukumu” na “usilaumu.” Tafsiri hizo humaanisha “usianze kuhukumu” na “usianze kulaumu.” Hata hivyo, waandishi wa Biblia waliandika amri hizo katika njeo ya wakati uliopo ili kuonyesha kitendo kinachoendelea. Kwa hiyo, matendo hayo yalikuwa yakiendelea lakini yalihitaji kukoma kabisa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki