Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Amehesabu “Nywele Zenyewe za Kichwa Chenu”
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Agosti 1
    • 6 Yesu alitoa mifano miwili ili kuwasaidia mitume wake kuelewa kwa nini hawapaswi kuogopa. Aliwaambia hivi: “Je, shomoro wawili hawauzwi kwa sarafu ya thamani ndogo? Na bado hakuna hata mmoja wao atakayeanguka chini bila Baba yenu kujua. Lakini nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote. Kwa hiyo msiogope: ninyi ni bora kuliko shomoro wengi.” (Mathayo 10:29-31) Ona kwamba Yesu alihusianisha kutoogopa majaribu na kuwa na uhakika kwamba Yehova anatujali sisi binafsi. Mtume Paulo alikuwa pia na uhakika huo. Aliandika: “Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani atakayekuwa dhidi yetu? Yeye ambaye hakujizuia hata Mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, kwa nini yeye pia pamoja naye hatatupa sisi kwa fadhili vitu vingine vyote?” (Waroma 8:31, 32) Hata ukikabili matatizo ya aina gani, wewe pia unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova anakujali kibinafsi maadamu unaendelea kuwa mshikamanifu kwake. Tutaelewa hilo vizuri zaidi tunapochunguza kwa undani himizo ambalo Yesu aliwapa mitume wake.

      Thamani ya Shomoro

      7, 8. (a) Shomoro walionwaje siku za Yesu? (b) Huenda ni kwa nini Mathayo 10:29 inatumia neno la Kigiriki linalorejelea “shomoro” wadogo?

      7 Mifano ya Yesu inaonyesha vizuri sana jinsi Yehova anavyomjali kila mmoja wa watumishi Wake. Kwanza fikiria mfano wa shomoro, au shore. Katika siku za Yesu, shomoro walikuwa chakula, lakini kwa kawaida walionwa kuwa ndege waharibifu kwa sababu waliharibu mimea. Shomoro walikuwa wengi sana na waliuzwa kwa bei ya chini sana hivi kwamba shomoro wawili walinunuliwa kwa senti zisizozidi tano za Marekani, kulingana na thamani ya leo. Mtu aliyenunua shomoro wanne aliongezewa shomoro mmoja kana kwamba shomoro huyo hakuwa na thamani yoyote!—Luka 12:6.

      8 Fikiria pia ukubwa wa ndege huyo. Hata shomoro aliyekomaa ni mdogo sana akilinganishwa na ndege wengine wengi. Hata hivyo, neno la Kigiriki ambalo limetafsiriwa “shomoro” katika Mathayo 10:29 linarejelea shomoro wadogo. Ni wazi kwamba Yesu alitaka mitume wake wafikirie ndege mdogo zaidi na mwenye thamani ndogo zaidi. Kama kichapo kimoja kinavyosema, “Yesu anamtaja ndege mdogo sana na hata anakazia udogo wa ndege huyo!”

      9. Mfano wa Yesu wa shomoro unakazia jambo gani muhimu sana?

      9 Mfano wa Yesu wa shomoro unakazia jambo muhimu sana: Vitu ambavyo havina thamani machoni pa wanadamu ni muhimu kwa Yehova Mungu. Yesu alikazia zaidi ukweli huo kwa kuongezea kwamba shomoro mdogo hawezi ‘kuanguka chini’ bila Yehova kujua.c Funzo ni wazi. Ikiwa Yehova Mungu anamjali ndege mdogo sana na mwenye thamani ndogo zaidi, basi anahangaikia hata zaidi hali ya mwanadamu ambaye ameamua kumtumikia!

  • Yehova Amehesabu “Nywele Zenyewe za Kichwa Chenu”
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Agosti 1
    • c Wasomi fulani wanasema kwamba kuanguka kwa shomoro chini huenda hakumaanishi kufa tu. Wanasema kwamba neno la lugha ya awali huenda linamaanisha ndege kutua chini ili kutafuta chakula. Ikiwa ni hivyo, basi ingemaanisha kwamba Mungu humkazia uangalifu na kumjali ndege huyo katika maisha ya kila siku, si wakati tu anapokufa.—Mathayo 6:26.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki