Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunapaswa Kusali kwa Mungu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012 | Februari
    • Yesu alisema: “Basi, ninyi msali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.

  • Tunapaswa Kusali kwa Mungu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012 | Februari
    • Mathayo 6:9

  • Tunapaswa Kusali kwa Mungu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012 | Februari
    • Ona kwamba Yesu alisema: “Basi, ninyi msali hivi.” Alimaanisha nini? Yesu hakumaanisha kwamba wafuasi wake wakariri au kurudia-rudia maneno yake kama kasuku. Alikuwa ametoka tu kuwakataza wasifanye hivyo. (Mathayo 6:7) Badala yake, sala yake inatoa somo kuhusu mambo ya kutanguliza​—mambo yaliyo muhimu, machoni pa Mungu, si machoni petu tu. Ili kujua ni mambo gani tunayopaswa kutanguliza, tunahitaji kuelewa maana ya maneno ya Yesu. Acheni basi tuchunguze maneno yake, moja baada ya lingine.

      Sala ya Kielelezo Yafafanuliwa

      “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.” Kwa kufaa Yesu alimwita Mungu “Baba” kwa sababu yeye ni mwenye upendo na anawalinda watoto wake, kama vile tu baba mzuri wa kibinadamu. Pia, yeye ana jina lake la kibinafsi—Yehova—​ambalo halipaswi kuchukuliwa kuwa jina la cheo sawa na majina yake mengine ya cheo, kama vile Mweza-Yote, Mungu, na Bwana.a (Zaburi 83:18) Lakini kwa nini jina la Mungu, ambalo linahusisha sifa yake, linahitaji kutakaswa, au kufanywa kuwa takatifu? Ni kwa sababu jina hilo limeshutumiwa na kuvunjiwa heshima.

      Watu fulani humlaumu Mungu kwa sababu ya majaribu yanayowapata, lakini huenda majaribu hayo yakasababishwa na wanadamu au huenda ni kwa sababu ya kuwa mahali pasipofaa wakati usiofaa. (Methali 19:3; Mhubiri 9:11) Wengine wamemshutumu Mungu kuwa ndiye anayesababisha misiba ya asili. Hata hivyo, Biblia inasema kwamba “Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote.” (Yakobo 1:13) Na dini nyingi zinafundisha kwamba Mungu anawaadhibu waovu kwa kuwatesa milele katika moto wa mateso, fundisho ambalo humchukiza sana Mungu mwenye upendo. (Yeremia 19:5; 1 Yohana 4:8) Waroma 6:23 inasema kwamba “mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo,” wala si kuteswa milele!b

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki