-
Mtumaini Yehova Kikamili Nyakati za TaabuMnara wa Mlinzi—2003 | Septemba 1
-
-
7, 8. (a) Yesu alionyeshaje kwamba anajua wanadamu wasio wakamilifu wana mwelekeo wa kuhangaikia vitu vya kimwili kupita kiasi? (Ona pia kielezi-chini.) (b) Yesu alitoa shauri gani lenye hekima kuhusu jinsi ya kuepuka kuwa na mahangaiko isivyofaa?
7 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu alishauri hivi: “Komeni kuhangaikia nafsi zenu kuhusu ni nini mtakula au ni nini mtakunywa, au juu ya miili yenu kuhusu ni nini mtavaa.”b (Mathayo 6:25) Yesu alijua kwamba kwa kawaida wanadamu wasio wakamilifu huhangaika kupata mahitaji ya lazima. Lakini tunawezaje ‘kukoma kuhangaikia’ vitu hivyo? Yesu alisema: “Fulizeni kutafuta kwanza ufalme.” Hata tuwe tunakabili matatizo gani, tunapaswa kuendelea kutanguliza ibada ya Yehova maishani. Tukifanya hivyo, Baba yetu wa mbinguni ‘atatuongezea’ mahitaji yetu yote ya kila siku. Kwa njia fulani, atatuandalia tunayohitaji.—Mathayo 6:33.
-
-
Mtumaini Yehova Kikamili Nyakati za TaabuMnara wa Mlinzi—2003 | Septemba 1
-
-
b Hangaiko linalotajwa hapa linasemekana kuwa ni “hofu inayosababisha wasiwasi ambao huondoa furaha yote maishani.” Tafsiri fulani zinasema “msisumbuke” au “msiwe na wasiwasi.” Lakini tafsiri hizo zinadokeza kwamba hatupaswi kuanza kuwa na wasiwasi au kusumbuka. Kichapo kimoja cha marejeo kinasema: “Njeo ya kitenzi cha Kigiriki iko katika hali ya kuamrisha sasa, ikionyesha amri ya kuacha kufanya jambo fulani ambalo tayari linaendelea.”
-