-
“Kristo Ni Nguvu ya Mungu”Mkaribie Yehova
-
-
Kisa kimoja chenye kugusa moyo kinasimuliwa kwenye Marko 7:31-37.
19 Pindi hiyo, umati mkubwa ulimfikia Yesu na kumletea wagonjwa wengi, naye akawaponya wote. (Mathayo 15:29, 30) Lakini Yesu alimshughulikia mtu mmoja kwa njia ya pekee sana. Mtu huyo alikuwa kiziwi asiyeweza kuongea. Yaelekea Yesu alitambua wasiwasi au aibu ya mtu huyo. Hivyo kwa kuonyesha kwamba anamjali, Yesu alimpeleka faraghani, mbali na umati. Kisha Yesu akamwonyesha ishara fulani ili kumjulisha jambo ambalo alitaka kufanya. Alitia “vidole vyake ndani ya masikio ya yule mtu na, baada ya kutema mate, akamgusa ulimi wake.”c (Marko 7:33) Halafu, Yesu akatazama juu mbinguni na kutweta kwa sala. Ni kana kwamba alikuwa akimwambia mtu huyo, ‘Muujiza ninaotaka kukufanyia unategemea nguvu za Mungu.’ Hatimaye, Yesu akasema: “Funguka.” (Marko 7:34) Basi, akayaponya masikio yake, kisha mtu huyo akaanza kuongea kama kawaida.
-
-
“Kristo Ni Nguvu ya Mungu”Mkaribie Yehova
-
-
c Kutema mate kulikuwa njia au ishara ya kuponya iliyokubaliwa na Wayahudi na Wasio Wayahudi. Na maandishi ya marabi yanataja tiba ya kutumia mate. Huenda Yesu alitema mate ili kumjulisha mtu huyo kwamba alitaka kumponya. Vyovyote iwavyo, Yesu hakuwa akitumia mate yake kama dawa ya asili.
-