-
“Nendeni Mkafanye Wanafunzi”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
12 Pia, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kuepuka mambo yasiyo ya lazima ambayo yangewakengeusha. Alisema hivi: “Msimkumbatie mtu yeyote mkimsalimu barabarani.” (Luka 10:4) Je, Yesu alikuwa akiwaambia wasipendezwe na watu wala kuwa wachangamfu? Hapana! Katika nyakati za Biblia, mara nyingi salamu zilitia ndani mambo mengi. Kwa kawaida, salamu zilitia ndani desturi fulani pamoja na mazungumzo marefu. Mtaalamu mmoja wa Biblia anasema: “Watu wa Mashariki hawakusalimiana kama tunavyofanya, yaani, kwa kuinama kidogo, au kwa kupeana mkono, bali walikumbatiana mara nyingi na kuinamisha kichwa na hata kusujudu. Yote hayo yalihitaji wakati mwingi.” Kwa kuwaambia wanafunzi wake wasisalimiane kulingana na desturi hizo, ni kana kwamba Yesu aliwaambia: “Mnapaswa kutumia wakati wenu vizuri kwa maana ujumbe mlio nao ni wa haraka.”b
-
-
“Nendeni Mkafanye Wanafunzi”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
b Wakati fulani, nabii Elisha alitoa maagizo kama hayo. Alipokuwa akimtuma mtumishi wake Gehazi kwenye nyumba ya mwanamke aliyefiwa na mwana wake, Elisha alisema: “Ukikutana na yeyote, usimsalimu.” (2 Wafalme 4:29) Mgawo huo ulihitaji kufanywa haraka, kwa hiyo hakupaswa kupoteza wakati.
-