Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuzaliwa Upya—Je, Ni Muhimu?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
    • Ona jinsi Yesu alivyokazia umuhimu wa kuzaliwa upya alipozungumza na Nikodemo. Alisema: “Mtu asipozaliwa tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3) Maneno “asipozaliwa tena” na “hawezi” yanaonyesha kwamba ni lazima mtu azaliwe upya. Kwa mfano: Mtu akisema, “Jua lisipowaka, hakuwezi kuwa na mwangaza wa mchana,” anamaanisha kwamba ni lazima jua liwake ili kuwe na mwangaza wa mchana. Vivyo hivyo, Yesu alisema kwamba kuzaliwa tena ni jambo la lazima kabisa ili kuuona Ufalme wa Mungu.

  • Kuzaliwa Upya—Je, Ni Uamuzi wa Mtu Binafsi?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
    • Unaposoma kwa makini maneno ya Yesu, utaona kuwa yeye hakufundisha kwamba mtu binafsi ndiye anayechagua kuzaliwa upya. Kwa nini tunasema hivyo? Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘kuzaliwa tena’ linaweza pia kutafsiriwa “kuzaliwa kutoka juu.”a Hivyo, mtu anazaliwa upya “kutoka juu,” yaani, “kutoka mbinguni,” au “kutoka kwa Baba.” (Yohana 19:11; Yakobo 1:17) Ndiyo, Mungu ndiye anayefanya mtu azaliwe upya.—1 Yohana 3:9.

  • Kuzaliwa Upya—Je, Ni Uamuzi wa Mtu Binafsi?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
    • a Katika Biblia kadhaa, Yohana 3:3 limetafsiriwa kwa njia hiyo. Kwa mfano, A Literal Translation of the Bible inasema: “Mtu asipozaliwa kutoka juu, hawezi kuuona Ufalme wa Mungu.”

  • Kuzaliwa Upya—Kusudi Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
    • Hata hivyo, ona vile Yesu mwenyewe alivyosema kuhusu kusudi la kuzaliwa upya. Alisema: “Mtu asipozaliwa tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3) Hivyo, mtu anahitaji kuzaliwa tena ili kuingia katika Ufalme wa Mungu, si ili kupata wokovu. Huenda wengine wakauliza, ‘Je, semi hizi mbili—kuingia katika Ufalme, na kupata wokovu—zinarejelea thawabu ileile?’ Hapana. Ili kuelewa tofauti, tutafikiria kwanza maana ya maneno “ufalme wa Mungu.”

      Ufalme ni aina fulani ya serikali. Kwa hiyo, maneno “ufalme wa Mungu” yanamaanisha “serikali ya Mungu.” Biblia inafundisha kwamba Yesu Kristo, “mwana wa binadamu,” ndiye Mfalme wa Ufalme wa Mungu na kwamba Kristo atatawala pamoja na wengine. (Danieli 7:1, 13, 14; Mathayo 26:63, 64) Isitoshe, maono fulani ambayo mtume Yohana alipokea yanafunua kwamba wale watakaotawala pamoja na Kristo wamechaguliwa “kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa,” nao “watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Ufunuo 5:9, 10; 20:6) Pia, Neno la Mungu linafunua kuwa wale watakaotawala wakiwa wafalme ni “kundi dogo” la watu 144,000 “ambao wamenunuliwa kutoka duniani.”—Luka 12:32; Ufunuo 14:1, 3.

      Ufalme wa Mungu uko wapi? “Ufalme wa Mungu” pia unaitwa “ufalme wa mbinguni,” jambo linaloonyesha kwamba Yesu na wafalme wenzake watatawala kutoka mbinguni. (Luka 8:10; Mathayo 13:11) Hivyo, Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni ambayo mtawala wake ni Yesu Kristo pamoja na kikundi cha watawala wenzake ambao wamechaguliwa kutoka kati ya wanadamu.

      Kwa hiyo, Yesu alimaanisha nini aliposema ni lazima mtu azaliwe tena ili “kuingia katika ufalme wa Mungu”? Alimaanisha kwamba mtu anahitaji kuzaliwa tena ili awe mtawala pamoja na Kristo mbinguni. Kwa wazi, kusudi la kuzaliwa upya ni kutayarisha kikundi cha wanadamu wachache kuwa watawala mbinguni.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki