-
Pumziko la Mungu Ni Nini?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
Kwanza, fikiria maneno ambayo Yesu aliwaambia wapinzani wake ambao walikasirika kwa sababu aliponya wagonjwa siku ya Sabato, jambo ambalo waliona kuwa ni kazi. Bwana aliwaambia hivi: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi mpaka sasa, na mimi ninaendelea kufanya kazi.” (Yoh. 5:16, 17) Alimaanisha nini? Yesu alishtakiwa kuwa alifanya kazi siku ya Sabato. Aliwajibu hivi: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi.” Kwa kweli, Yesu alikuwa akiwaambia hivi wapinzani wake: ‘Mimi na Baba yangu tunafanya kazi ileile. Kwa kuwa Baba yangu anaendelea kufanya kazi wakati wa Sabato yake ya maelfu ya miaka, ninaruhusiwa pia kuendelea kufanya kazi hata siku ya Sabato.’ Hivyo, Yesu alimaanisha kwamba kuhusiana na dunia, siku ya Sabato kuu ya Mungu ya kupumzika, yaani, siku ya saba, ilikuwa bado inaendelea katika siku za Yesu.a
-
-
Pumziko la Mungu Ni Nini?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
5. Ni nini lililokuwa kusudi la siku ya saba, na kusudi hilo litatimia kabisa wakati gani?
5 Ili kujibu swali hilo, ni lazima tukumbuke kusudi la siku ya saba. Andiko la Mwanzo 2:3 linaeleza hivi: “Mungu akaibariki siku ya saba na kuifanya takatifu.” Siku hiyo ‘ilifanywa kuwa takatifu,’ yaani, ilitakaswa, au iliwekwa kando na Yehova ili kukamilisha kusudi lake. Kusudi hilo ni kwamba dunia ikaliwe na wanaume na wanawake watiifu ambao wataitunza na kutunza viumbe wote walio hai. (Mwa. 1:28) Yehova Mungu na Yesu Kristo, ambaye ni “Bwana wa Sabato,” ‘wameendelea kufanya kazi mpaka sasa’ ili watimize kusudi hilo. (Mt. 12:8)
-
-
Pumziko la Mungu Ni Nini?Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
a Makuhani na Walawi walifanya kazi za hekalu siku ya Sabato, hata hivyo ‘walibaki bila hatia.’ Akiwa kuhani mkuu wa hekalu kuu la kiroho la Mungu, Yesu angeweza pia kutimiza mgawo wake wa kiroho bila kuogopa kuvunja Sabato.—Mt. 12:5, 6.
-