-
Usitawi wa Muundo wa TengenezoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Lakini je, Matendo 14:23 halikuonyesha kwamba wazee katika makutaniko walikuwa wamewekwa kwenye cheo kwa ‘kunyoosha mkono,’ kama katika kupiga kura? Ya kwanza kati ya makala hizo za Mnara wa Mlinzi yenye kichwa “Tengenezo” ilikiri kwamba andiko hilo lilikuwa limeeleweka kimakosa wakati uliopita. Haikuwa kwa ‘kunyoosha mkono’ upande wa washiriki wote wa kutaniko kwamba kuweka rasmi kulikuwa kumefanywa miongoni mwa Wakristo wa karne ya kwanza. Badala ya hivyo, ilionyeshwa, mitume na wale waliopewa mamlaka nao ndio ‘walionyoosha mikono yao.’ Hilo lilifanywa si kwa kushiriki kupiga kura katika kutaniko bali kwa kuweka mikono yao juu ya watu mmoja-mmoja waliostahili. Hiyo ilikuwa ishara ya uthibitisho, kibali, au uwekaji rasmi.k Nyakati nyingine makutaniko ya Kikristo ya mapema yalipendekeza wanaume waliostahili, lakini uteuzi au kibali cha mwisho vilitolewa na mitume, ambao walikuwa wamepewa utume moja kwa moja na Kristo, au kibali kilitolewa na wale waliopewa mamlaka na mitume. (Mdo. 6:1-6) Mnara wa Mlinzi lilivuta uangalifu kwenye uhakika wa kwamba ni katika barua kwa waangalizi wenye daraka tu (Timotheo na Tito) kwamba mtume Paulo, chini ya mwelekezo wa roho takatifu, alitoa maagizo waangalizi wawekwe. (1 Tim. 3:1-13; 5:22; Tito 1:5) Hakuna yoyote ya barua zilizopuliziwa ambazo zilipelekwa kwenye makutaniko zilizokuwa na maagizo kama hayo.
-
-
Usitawi wa Muundo wa TengenezoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
k Kitenzi cha Kigiriki khei·ro·to·neʹo kifafanuliwapo kuwa chamaanisha tu ‘kuchagua kwa kunyoosha mkono,’ hilo hushindwa kuangalia maana ya baadaye ya neno hilo. Hivyo, A Greek-English Lexicon, ya Liddell na Scott, iliyohaririwa na Jones na McKenzie na kuchapwa upya katika 1968, hufafanua neno hilo kuwa likimaanisha “kunyoosha mkono, kwa kusudi la kutoa kura ya mtu katika kusanyiko . . . II. c. acc. pers. [kwa kuhusu mtu], kuchagua, [kwa kufaa] kwa wonyesho wa mikono . . . b. baadaye, kijumla, kuweka rasmi, . . . kuweka rasmi kwenye cheo Kanisani, [pre·sby·teʹrous] Act. Ap. [Matendo ya Mitume] 14.23.” Utumizi huo wa baadaye ulikuwa ukiendelea katika siku za mitume; neno hilo lilitumiwa katika maana hiyo na mwanahistoria wa Kiyahudi Yosefo wa karne ya kwanza katika Jewish Antiquities, Buku 6, sura ya 4, fungu 2, na sura ya 13, fungu 9. Muundo wa kisarufi wenyewe wa Matendo 14:23 katika Kigiriki cha awali huonyesha kwamba Paulo na Barnaba ndio waliofanya yale yaliyoelezwa humo.
-