Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu na Kaisari
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Mei 1
    • 11. Paulo aliwashaurije Wakristo jinsi ya kushughulika na watawala wa kilimwengu?

      11 Ilikuwa kupatana na hiyo kanuni kwamba, muda uzidio kidogo miaka 20 baada ya kifo cha Kristo, mtume Paulo aliwaambia Wakristo katika Roma: “Kila nafsi na iwe katika ujitiisho kwa mamlaka zilizo kubwa.” (Waroma 13:1, NW) Karibu miaka kumi baadaye, muda mfupi kabla ya kufungwa kwake kwa mara ya pili na kuuawa katika Roma, Paulo alimwandikia Tito hivi: “Uwakumbushe watu [Wakristo wa Krete] kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.”—Tito 3:1, 2.

      Uelewevu Wenye Kuendelea Juu ya “Mamlaka Zilizo Kubwa”

      12. (a) Charles Taze Russell alikuwa na maoni gani juu ya msimamo ufaao wa Mkristo kuhusu mamlaka za kiserikali? (b) Kuhusu kutumikia katika jeshi, ni maoni gani yaliyotofautiana ambayo Wakristo watiwa-mafuta walikuwa nayo wakati wa Vita ya Ulimwengu 1?

      12 Mapema kama 1886, Charles Taze Russell aliandika katika kitabu The Plan of the Ages: “Wala Yesu wala Mitume hawakuingilia watawala wa kidunia kwa njia yoyote. . . . Walifundisha Kanisa kutii sheria, na kustahi wale walio mamlakani kwa sababu ya cheo chao, . . . walipe kodi zao zilizowekwa, na ila tu zilipopingana na sheria za Mungu (Mdo. 4:19; 5:29) hawakuwa wapinge sheria yoyote iliyowekwa. (Rum. 13:1-7; Mt. 22:21) Yesu na Mitume na kanisa la mapema wote walikuwa watii-sheria, ingawa wao walikuwa tofauti na serikali za ulimwengu huu nao hawakushiriki katika hizo.” Kitabu hiki kilitambulisha kwa usahihi “mamlaka za juu,” au “mamlaka zilizo kubwa,” zinazotajwa na mtume Paulo, kuwa mamlaka za kiserikali za kibinadamu. (Warumi 13:1, King James Version) Katika 1904 kitabu The New Creation kilisema kwamba Wakristo wa kweli “wapaswa kuwa miongoni mwa watu wenye kutii sheria zaidi wa wakati huu—si wachochezi, si wagomvi, si watafuta-makosa.” Jambo hilo lilieleweka kwa wengine kumaanisha unyenyekeo kamili kwa mamlaka, hata kufikia hatua ya kukubali utumishi katika jeshi wakati wa Vita ya Ulimwengu 1. Hata hivyo wengine waliona utumishi wa jeshi kuwa kinyume cha taarifa hii ya Yesu: “Wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.” (Mathayo 26:52) Bila shaka, uelewevu wazi zaidi wa unyenyekeo wa Kikristo kwa mamlaka zilizo kubwa ulihitajika.

      13. Ni badiliko gani katika uelewevu wa utambulisho wa mamlaka za juu lililotolewa katika 1929, na hilo lilithibitikaje kuwa lenye manufaa?

      13 Katika 1929, wakati sheria za serikali mbalimbali zilipoanza kukataza mambo aliyoyaamuru Mungu au kudai mambo ambayo sheria ya Mungu ilikataza, ilihisiwa kwamba mamlaka za juu lazima zilikuwa ni Yehova Mungu na Yesu Kristo.b Huo ulikuwa ndio uelewevu wa watumishi wa Yehova katika kipindi chenye umaana cha kabla ya na wakati wa Vita ya Ulimwengu 2 na kuendelea hadi ile Vita Baridi, iliyokuwa yenye kuogofywa pia na yenye utayari kijeshi. Kwa kutazama nyuma, ni wazi kwamba maoni hayo, ambayo yalitukuza ukuu kupita wote wa Yehova na Kristo wake, yalisaidia watu wa Mungu kudumisha msimamo usioridhiana kamwe katika kipindi hicho chote kigumu.

      Unyenyekeo Husianifu

      14. Nuru iliyoongezeka iliangazwaje kwenye Warumi 13:1, 2 na maandiko yanayohusiana nalo katika 1962?

      14 Katika 1961 New World Translation of the Holy Scriptures ilikamilishwa. Utayarishaji wayo ulihitaji uchunguzi wa kina sana wa lugha ya Maandiko. Tafsiri sahihi kabisa ya maneno ambayo hayakutumiwa katika Warumi sura ya 13 pekee bali yaliyotumiwa pia katika mafungu kama Tito 3:1, 2 na 1 Petro 2:13, 17 yalidhihirisha kwamba usemi “mamlaka zilizo kubwa” haukurejezea Mamlaka Kuu Kupita Zote, Yehova, na Mwanaye, Yesu, bali ulirejezea mamlaka za kiserikali za kibinadamu. Mwishoni-mwishoni mwa 1962, makala zilichapishwa katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) zilizotoa maelezo sahihi ya Warumi sura ya 13 na pia kuandaa mwono wa wazi kuliko ule wa wakati wa C. T. Russell. Makala hizi zilisema kwamba utii wa Kikristo kwa mamlaka hauwezi kuwa kamili. Ni lazima uwe husianifu, ili usifanye watumishi wa Mungu wapingane na sheria za Mungu. Makala zaidi za Mnara wa Mlinzi zimekazia jambo hili muhimu.c

      15, 16. (a) Uelewevu mpya wa Warumi sura ya 13 ulitokeza maoni gani yenye usawaziko mzuri zaidi? (b) Ni maswali gani yanayobaki kujibiwa?

      15 Ufunguo huu wa uelewevu sahihi wa Warumi sura ya 13 umewezesha watu wa Yehova kusawazisha staha inayostahili mamlaka za kisiasa na msimamo usioridhiana juu ya kanuni za Kimaandiko zilizo muhimu. (Zaburi 97:11; Yeremia 3:15) Umewawezesha wawe na maoni yafaayo juu ya uhusiano wao na Mungu na shughuli zao na Serikali. Umehakikisha kwamba huku wakimpa Kaisari yaliyo ya Kaisari, hawapuuzi kumpa Mungu yaliyo ya Mungu.

  • Mungu na Kaisari
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Mei 1
    • Kwa kupendeza, katika kufafanua Warumi sura ya 13, Profesa F. F. Bruce aandika: “Ni wazi katika muktadha wa [Warumi 13], kama ilivyo na muktadha wa ujumla wa maandiko ya kimitume, kwamba serikali yaweza kwa halali kudai utii kutokana tu na viwango vya makusudi ambayo hiyo serikali imewekewa kimungu—hasa, serikali haiwezi kukinzwa tu, bali ni lazima ikinzwe inapodai utii unaopaswa kuwa wa Mungu pekee.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki