-
Jifunze na Uwafundishe Wengine Maadili ya KikristoMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
Wewe, unayehubiri ‘Usiibe,’ je, wewe huiba? Wewe, unayesema ‘Usifanye uzinzi,’ je, wewe hufanya uzinzi? Wewe, unayeonyesha chukio kubwa la sanamu, je, wewe hupokonya mahekalu?
-
-
Jifunze na Uwafundishe Wengine Maadili ya KikristoMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
7 Kwa kutumia maswali hayo yasiyohitaji majibu, Paulo alionyesha makosa mawili yaliyotajwa katika Amri Kumi: Usiibe na usizini. (Kutoka 20:14, 15) Wayahudi fulani wa siku za Paulo walijivunia kuwa na Sheria ya Mungu. ‘Walifundishwa kwa mdomo kutokana na Sheria na wakashawishwa kwamba walikuwa viongozi wa walio vipofu, na nuru kwa wale walio katika giza, walimu wa vitoto.’ (Waroma 2:17-20) Hata hivyo, wengine walikuwa wanafiki kwa sababu walikuwa wakiiba au kuzini kisiri. Matendo hayo hayakuiheshimu Sheria wala kumheshimu Mtungaji wa Sheria hiyo aliye mbinguni. Unaweza kuona kwamba hawakustahili kuwafundisha wengine kwa kuwa wao wenyewe hawakuwa wakijifunza.
8. Huenda Wayahudi fulani wa siku za Paulo ‘waliyapokonya mahekalu’ kwa njia gani?
8 Paulo alizungumza kuhusu kupokonya mahekalu. Je, Wayahudi fulani walifanya hivyo kihalisi? Paulo alikuwa akimaanisha nini? Kulingana na habari chache zinazopatikana katika andiko hilo, hatuwezi kusema kwa uhakika jinsi Wayahudi fulani ‘walivyopokonya mahekalu.’ Mapema kidogo, karani wa jiji la Efeso alisema kwamba Paulo na wenzake hawakuwa “wapokonya-mahekalu,” jambo linalodokeza kwamba watu fulani walifikiri kwamba Wayahudi walipokonya mahekalu. (Matendo 19:29-37) Je, walikuwa wakitumia au kuuza vitu fulani vya thamani kutoka kwa mahekalu ya wapagani ambayo yalikuwa yameporwa na watekaji au wafuasi shupavu wa dini ya Kiyahudi? Kulingana na Sheria ya Mungu, dhahabu na fedha iliyotengeneza sanamu ingepaswa kuharibiwa, wala si kuchukuliwa kwa matumizi ya kibinafsi. (Kumbukumbu la Torati 7:25)a Kwa hiyo huenda Paulo alikuwa akizungumza kuhusu Wayahudi waliopuuza amri ya Mungu na kutumia au kufaidika na vitu vilivyotoka katika mahekalu ya wapagani.
9. Ni mambo gani yasiyofaa yaliyofanywa hekaluni huko Yerusalemu ambayo huenda yangekuwa sawa na kupokonya hekalu?
9 Kwa upande mwingine, Josephus alitaja kashfa nyingine huko Roma iliyosababishwa na Wayahudi wanne wakioongozwa na mwalimu wa Sheria. Wayahudi hao wanne walimshawishi mwanamke Mroma, aliyekuwa amegeuzwa imani akawa mfuasi wa dini ya Kiyahudi, achange dhahabu na vitu vingine vya thamani kwenye hekalu huko Yerusalemu. Walipopata vitu hivyo kutoka kwake, walivitumia kujitajirisha. Jambo hilo lilikuwa sawa na kupokonya hekalu.b Wengine walikuwa wakipokonya hekalu la Mungu kwa kutoa dhabihu zenye kasoro na kuendeleza biashara yenye pupa hekaluni, hivyo kulifanya kuwa “pango la wapokonyaji.”—Mathayo 21:12, 13; Malaki 1:12-14; 3:8, 9.
-
-
Jifunze na Uwafundishe Wengine Maadili ya KikristoMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
a Ingawa Josephus anaonyesha kwamba Wayahudi waliheshimu vitu vitakatifu, yeye aliirudia sheria ya Mungu kwa kusema hivi: “Mtu yeyote na asikufuru miungu ambayo majiji mengine huabudu, wala kupokonya mahekalu ya kigeni, wala kuchukua vitu vya thamani ambavyo vimewekwa wakfu kwa mungu yeyote yule.” (Italiki ni zetu.)—Jewish Antiquities, Kitabu cha 4, sura ya 8, fungu la 10.
-