Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usitenganishe Kile Ambacho Mungu Ameunganisha
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 1
    • Vivyo hivyo waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Yeye anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo, kama vile Kristo pia anavyolitendea kutaniko.

  • Usitenganishe Kile Ambacho Mungu Ameunganisha
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 1
    • Waefeso 5:25, 28, 29,

  • Usitenganishe Kile Ambacho Mungu Ameunganisha
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 1
    • Inamaanisha Nini Kumtunza Mke Wako?

      10. Mume anaweza kuonyesha jinsi gani kwamba anamthamini mke wake?

      10 Ikiwa unamthamini mke wako, utamtunza sana kwa sababu unampenda. Unaweza kufanya hivyo kwa njia mbalimbali. Kwanza, tumia wakati wa kutosha pamoja na mwenzi wako. Ukimpuuza mke wako kuhusiana na jambo hilo, upendo wake kwako unaweza kupoa. Pia, fikiria hili, inapohusu wakati na uangalifu huenda kile ambacho unadhani mke wako anahitaji kisiwe kile anachohitaji. Haitoshi tu kusema kwamba unamthamini mwenzi wako. Ni lazima mke wako ahisi kwamba anathaminiwa. Paulo aliandika hivi: “Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali ile ya yule mtu mwingine.” (1 Wakorintho 10:24) Ukiwa mume mwenye upendo, unapaswa kujitahidi kuelewa mahitaji kamili ya mke wako.—Wafilipi 2:4.

      11. Jinsi mume anavyomtendea mke wake kunaweza kuwa na matokeo gani juu ya uhusiano wake pamoja na Mungu na kutaniko?

      11 Njia nyingine ya kuonyesha kwamba unamthamini mke wako ni kumtendea kwa wororo, kwa maneno na kwa matendo. (Methali 12:18) Paulo aliwaandikia hivi Wakolosai: “Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.” (Wakolosai 3:19) Kulingana na kitabu kimoja, sehemu ya mwisho ya maneno ya Paulo inaweza kutafsiriwa hivi “usimtendee mke kama mfanyakazi wa nyumbani” au “usimfanye mke kuwa mtumwa.” Bila shaka, mume ambaye ni mkatili, iwe hadharani au faraghani, anaonyesha kwa kweli kwamba hamthamini mke wake. Mume anayemtendea mke wake kwa ukali, anaweza kuharibu uhusiano wake pamoja na Mungu. Mtume Petro aliwaandikia waume hivi: “Enyi waume, endeleeni kukaa nao [wake zenu] vivyo hivyo kulingana na ujuzi, mkiwapa heshima kama chombo dhaifu zaidi, yaani, mwanamke, kwa kuwa ninyi pia ni warithi pamoja nao wa pendeleo lisilostahiliwa la uzima, kusudi sala zenu zisizuiwe.”c—1 Petro 3:7.

      12. Mume Mkristo anaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Yesu alivyolitendea kutaniko la Kikristo?

      12 Usipuuze upendo wa mke wako. Mhakikishie kwamba bado unaendelea kumpenda. Yesu aliwawekea waume Wakristo mfano kupitia jinsi alivyolitendea kutaniko la Kikristo. Alikuwa mwororo, mwenye fadhili, na mwenye kusamehe, hata wafuasi wake waliporudia-rudia kuonyesha sifa zisizopendeza. Hivyo, Yesu angeweza kuwaambia wengine hivi: “Njooni kwangu, . . . kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu.” (Mathayo 11:28, 29) Mume Mkristo anayemwiga Yesu anamtendea mke wake kama Yesu alivyolitendea kutaniko. Mwanamume ambaye kwa kweli anamthamini mke wake, na kuonyesha hivyo kwa maneno na matendo, atakuwa chanzo cha burudisho la kweli kwa mke wake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki