-
“Alitupenda Sisi Kwanza”Mkaribie Yehova
-
-
“Mungu Ni Upendo”
15. Biblia inasema nini kuhusu sifa ya Yehova ya upendo, na kwa nini usemi huo ni wa pekee sana? (Ona pia kielezi-chini.)
15 Biblia inasema jambo fulani la pekee kuhusu upendo ambalo haisemi kuhusu zile sifa nyingine kuu za Yehova. Maandiko hayasemi kwamba Mungu ni nguvu wala hayasemi kwamba Mungu ni haki au hata Mungu ni hekima. Ana sifa hizo, yeye ndiye chanzo chake, na hana kifani katika sifa hizo tatu. Hata hivyo, kuhusu sifa ya nne, Biblia inasema jambo fulani la pekee sana: “Mungu ni upendo.”b (1 Yohana 4:8) Hilo lamaanisha nini?
16-18. (a) Kwa nini Biblia inasema kwamba “Mungu ni upendo”? (b) Kati ya viumbe wote duniani, kwa nini mwanadamu ni mfano unaofaa wa sifa ya Yehova ya upendo?
16 Usemi “Mungu ni upendo” haulingani na usemi, “Mungu ni sawa na upendo.” Hatuwezi kamwe kugeuza usemi huo na kusema “upendo ni Mungu.” Yehova si sifa fulani tu. Ana utu, na mbali na upendo ana hisia na sifa nyingi mbalimbali. Hata hivyo, Yehova ana upendo mwingi sana. Kichapo kimoja cha marejeo kinasema hivi kuhusu mstari huo: “Upendo ni utu au sifa ya asili ya Mungu.” Kwa ujumla, tunaweza kulifikiria jambo hilo kwa njia hii: Nguvu za Yehova humwezesha kutenda. Haki na hekima yake humwongoza kutenda. Lakini upendo wa Yehova humchochea kutenda. Naye sikuzote hutumia sifa nyingine zote kupatana na upendo wake.
17 Mara nyingi imesemwa kwamba Yehova ni wonyesho halisi wa upendo. Kwa hiyo, tukitaka kujifunza kuhusu upendo unaotegemea kanuni, ni lazima tujifunze kumhusu Yehova. Bila shaka, wanadamu pia wana sifa hiyo yenye kupendeza. Lakini kwa nini wanadamu wana sifa hiyo? Wakati wa uumbaji, Yehova alimwambia hivi Mwanaye: “Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu.” (Mwanzo 1:26) Kati ya viumbe wote duniani, ni wanaume na wanawake tu wanaoweza kupenda na hivyo kumwiga Baba yao wa mbinguni. Kumbuka kwamba Yehova alitumia viumbe mbalimbali kuwa mifano ya sifa zake kuu. Hata hivyo, Yehova alimtumia mwanadamu—kiumbe bora zaidi duniani—kuwa mfano wa sifa Yake kuu zaidi ya upendo.—Ezekieli 1:10.
-
-
“Alitupenda Sisi Kwanza”Mkaribie Yehova
-
-
b Maandiko mengine yanatumia semi kama hizo. Kwa mfano, “Mungu ni nuru” na “Mungu . . . ni moto unaokula kabisa.” (1 Yohana 1:5; Waebrania 12:29) Lakini semi hizo zinapasa kuonwa kuwa milinganisho (sitiari), kwa kuwa zinamlinganisha Yehova na vitu vya asili. Yehova ni kama nuru, kwa kuwa yeye ni mtakatifu na mwadilifu. Hana “giza” wala uchafu wowote. Naye anaweza kulinganishwa na moto kwa sababu ya nguvu zake za kuangamiza.
-