-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“‘Na mimi nitafanya mashahidi wangu wawili watoe unabii siku elfu moja mia mbili na sitini wakiwa wamevalia nguo za magunia.’
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
11. Ilimaanisha nini kwa Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu kutoa unabii “wakiwa wamevalia nguo za magunia”?
11 Wakristo hawa wapakwa-mafuta waaminifu walihitaji sifa ya uvumilivu, kwa kuwa walipaswa kutoa unabii “wakiwa wamevalia nguo za magunia.” Hiyo ilimaanisha nini? Katika nyakati za Biblia mara nyingi nguo ya gunia ilifananisha maombolezo. Kuivaa kulikuwa ishara ya kwamba mtu alikuwa ameshushwa katika huzuni au dhiki. (Mwanzo 37:34; Ayubu 16:15, 16; Ezekieli 27:31, NW) Nguo ya gunia ilishirikishwa na jumbe za maombolezo za maangamizi au huzuni ambazo manabii wa Mungu walipaswa kupigia mbiu. (Isaya 3:8, 24-26; Yeremia 48:37; 49:3) Kuvaa nguo ya gunia kungeweza kuonyesha unyenyekevu au toba kwa sababu ya onyo la kimungu. (Yona 3:5) Nguo za Magunia zenye kuvaliwa na mashahidi wawili huonekana kuwa zinaonyesha uvumilivu wa unyenyekevu katika kutangaza hukumu za Yehova. Wao walikuwa mashahidi wakipiga mbiu ya siku yake ya kisasi ambayo ingeleta pia maombolezo kwa mataifa hayo.—Kumbukumbu 32:41-43.
12. Ni kwa nini kipindi cha wakati ambacho jiji takatifu lingekanyagwa chini ya nyayo huonekana kuwa halisi?
12 Jamii ya Yohana ilipaswa ihubiri ujumbe huu kwa wakati dhahiri uliotajwa: siku 1,260, au miezi 42, urefu ule ule wa wakati ambao jiji takatifu lingekanyagwa chini ya nyayo. Kipindi hiki kinaonekana kuwa halisi, kwa maana kinasemwa kwa njia mbili tofauti, kwanza kwa miezi na kisha kwa siku. Kwa kuongezea, mwanzoni mwa siku ya Bwana, kulikuwako wakati uliotiwa alama wa miaka mitatu na nusu ambao magumu yaliyowapata watu wa Mungu yalilingana na matukio yaliyotolewa unabii hapa—kuanzia Desemba 1914 na kuendelea mpaka Juni 1918. (Ufunuo 1:10) Wao walihubiri ujumbe wa “nguo za magunia” kuhusu hukumu za Yehova juu ya Jumuiya ya Wakristo na ulimwengu.
13. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba Wakristo wapakwa-mafuta walifananishwa na mashahidi wawili? (b) Ni unabii gani wa Zekaria ambao tunakumbushwa na Yohana kuwaita mashahidi wawili “mizeituni miwili na vinara vya taa viwili”?
13 Uhakika wa kwamba wao walifananishwa na mashahidi wawili unatuthibitishia kwamba ujumbe wao ni sahihi na una msingi mzuri. (Linga Kumbukumbu 17:6; Yohana 8:17, 18.)
-