Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 17
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Kumbukumbu la Torati—Yaliyomo

      • Dhabihu zisiwe na kasoro (1)

      • Kushughulikia uasi imani (2-7)

      • Kuamua kesi ngumu (8-13)

      • Maagizo kwa ajili ya mfalme atakayetawala (14-20)

        • Mfalme aandike nakala ya Sheria (18)

Kumbukumbu la Torati 17:1

Marejeo

  • +Law 22:20; Kum 15:21; Mal 1:8

Kumbukumbu la Torati 17:2

Marejeo

  • +Kum 4:23; 13:6-9

Kumbukumbu la Torati 17:3

Marejeo

  • +Kum 4:19
  • +Kum 13:12-15

Kumbukumbu la Torati 17:4

Marejeo

  • +Yoh 7:51

Kumbukumbu la Torati 17:5

Marejeo

  • +Kum 13:6, 10

Kumbukumbu la Torati 17:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kinywa cha.”

Marejeo

  • +Mt 18:16; Yoh 8:17; 1Ti 5:19; Ebr 10:28
  • +Hes 35:30; Kum 19:15

Kumbukumbu la Torati 17:7

Marejeo

  • +Kum 13:5; 1Ko 5:13

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” uku. 213

Kumbukumbu la Torati 17:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kumwaga damu.”

Marejeo

  • +Hes 35:11
  • +Kum 12:5; 1Fa 3:16, 28; Zb 122:2, 5

Kumbukumbu la Torati 17:9

Marejeo

  • +1Sa 7:15, 16
  • +Kum 19:17; 21:5

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ulimwengu Usio na Vita, uku. 11

Kumbukumbu la Torati 17:11

Marejeo

  • +Mal 2:7
  • +Kum 5:32; 12:32

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ulimwengu Usio na Vita, uku. 11

Kumbukumbu la Torati 17:12

Marejeo

  • +Met 11:2; Ebr 10:28
  • +Kum 13:5; 1Ko 5:13

Kumbukumbu la Torati 17:13

Marejeo

  • +Kum 13:11; 19:20

Kumbukumbu la Torati 17:14

Marejeo

  • +1Sa 8:5, 20; 10:19

Kumbukumbu la Torati 17:15

Marejeo

  • +1Sa 9:17; 10:24; 16:12, 13

Kumbukumbu la Torati 17:16

Marejeo

  • +Kum 20:1; 2Sa 8:4; Zb 20:7; Met 21:31
  • +Isa 31:1

Kumbukumbu la Torati 17:17

Marejeo

  • +1Fa 11:1-3; Ne 13:26
  • +Ayu 31:24, 28; 1Ti 6:9

Kumbukumbu la Torati 17:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hati ya kukunjwa.”

Marejeo

  • +Kum 31:9, 26; 2Fa 22:8

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    3/15/2007, uku. 20

    5/1/1995, kur. 12-13

    “Kila Andiko,” uku. 36

  • Fahirishi ya Machapisho

    w07 3/15 20

Kumbukumbu la Torati 17:19

Marejeo

  • +2Nya 34:18
  • +Zb 1:2; 119:97

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    6/15/2002, kur. 12-17

    10/1/2000, uku. 8

    5/1/1995, kur. 12-13

  • Fahirishi ya Machapisho

    w02 6/15 12-17; w00 10/1 8

Kumbukumbu la Torati 17:20

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    5/1/1995, kur. 12-13

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

Kum. 17:1Law 22:20; Kum 15:21; Mal 1:8
Kum. 17:2Kum 4:23; 13:6-9
Kum. 17:3Kum 4:19
Kum. 17:3Kum 13:12-15
Kum. 17:4Yoh 7:51
Kum. 17:5Kum 13:6, 10
Kum. 17:6Mt 18:16; Yoh 8:17; 1Ti 5:19; Ebr 10:28
Kum. 17:6Hes 35:30; Kum 19:15
Kum. 17:7Kum 13:5; 1Ko 5:13
Kum. 17:8Hes 35:11
Kum. 17:8Kum 12:5; 1Fa 3:16, 28; Zb 122:2, 5
Kum. 17:91Sa 7:15, 16
Kum. 17:9Kum 19:17; 21:5
Kum. 17:11Mal 2:7
Kum. 17:11Kum 5:32; 12:32
Kum. 17:12Met 11:2; Ebr 10:28
Kum. 17:12Kum 13:5; 1Ko 5:13
Kum. 17:13Kum 13:11; 19:20
Kum. 17:141Sa 8:5, 20; 10:19
Kum. 17:151Sa 9:17; 10:24; 16:12, 13
Kum. 17:16Kum 20:1; 2Sa 8:4; Zb 20:7; Met 21:31
Kum. 17:16Isa 31:1
Kum. 17:171Fa 11:1-3; Ne 13:26
Kum. 17:17Ayu 31:24, 28; 1Ti 6:9
Kum. 17:18Kum 31:9, 26; 2Fa 22:8
Kum. 17:192Nya 34:18
Kum. 17:19Zb 1:2; 119:97
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Kumbukumbu la Torati 17:1-20

Kumbukumbu la Torati

17 “Usimtolee Yehova Mungu wako dhabihu ya ng’ombe dume au kondoo mwenye kasoro au mwenye tatizo lolote, kwa sababu jambo hilo litakuwa chukizo kwa Yehova Mungu wako.+

2 “Ikiwa mwanamume au mwanamke atapatikana miongoni mwenu, katika mojawapo ya majiji ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, aliye na mazoea ya kufanya uovu machoni pa Yehova Mungu wenu na kuvunja agano lake,+ 3 naye anapotoka na kuabudu miungu mingine na kuiinamia miungu hiyo au jua au mwezi au jeshi lote la mbinguni,+ jambo ambalo sijaamuru,+ 4 ukiambiwa au kusikia habari hiyo, unapaswa kuchunguza jambo hilo kikamili. Ikithibitishwa ni kweli+ kwamba jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa katika Israeli, 5 utamtoa nje ya malango ya jiji lenu mwanamume au mwanamke ambaye amefanya uovu huo, na lazima mwanamume au mwanamke huyo auawe kwa kupigwa mawe.+ 6 Kwa ushahidi wa* mashahidi wawili au watatu+ yule anayepaswa kufa atauawa. Hapaswi kuuawa kwa ushahidi wa shahidi mmoja.+ 7 Mikono ya mashahidi inapaswa kuwa ya kwanza kumuua, kisha mikono ya watu wengine wote. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.+

8 “Ikiwa kesi ambayo ni ngumu sana kwenu kuamua inatokea katika mojawapo ya majiji yenu, iwe ni kesi ya kuua*+ au dai la kisheria limezushwa, au tendo la ukatili limefanywa, au mizozo mingine, mnapaswa kwenda mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua.+ 9 Nendeni kwa makuhani Walawi na kwa mwamuzi+ anayehudumu wakati huo, muwapelekee mashtaka yenu, nao watafanya uamuzi.+ 10 Kisha mnapaswa kutenda kulingana na uamuzi watakaofanya mahali hapo palipochaguliwa na Yehova. Muwe waangalifu kufanya mambo yote wanayowaagiza. 11 Mnapaswa kutenda kulingana na sheria watakayowaonyesha na kulingana na uamuzi watakaowatangazia.+ Msigeuke na kuacha uamuzi watakaofanya, na kwenda kulia au kushoto.+ 12 Mtu anayetenda kwa kimbelembele kwa kukataa kumsikiliza kuhani anayemhudumia Yehova Mungu wenu au kukataa kumsikiliza mwamuzi ni lazima afe.+ Ni lazima mwondoe uovu katika Israeli.+ 13 Basi watu wote watasikia na kuogopa, nao hawatatenda tena kwa kimbelembele.+

14 “Mtakapoingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, mkaimiliki na kuishi humo, nanyi mseme, ‘Na tumweke mfalme juu yetu kama mataifa yote yanayotuzunguka,’+ 15 mnapaswa kumweka mfalme ambaye Yehova Mungu wenu atamchagua.+ Mnapaswa kumchagua mfalme kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Hamruhusiwi kumweka mfalme ambaye ni mgeni, ambaye si ndugu yenu. 16 Hata hivyo, hapaswi kujipatia farasi wengi+ au kuwafanya watu warudi Misri kuchukua farasi wengi zaidi,+ kwa kuwa Yehova aliwaambia hivi: ‘Msirudi huko tena kamwe kupitia njia hii.’ 17 Wala hapaswi kuwa na wake wengi, ili moyo wake usipotoke;+ wala hapaswi kujipatia fedha na dhahabu nyingi sana.+ 18 Atakapoketi kwenye kiti cha ufalme wake, ni lazima ajiandikie kwenye kitabu* nakala ya Sheria hii, kwa kutumia nakala inayowekwa na makuhani Walawi.+

19 “Anapaswa kubaki nacho, naye lazima akisome sikuzote za maisha yake,+ ili ajifunze kumwogopa Yehova Mungu wake na kushika maneno yote ya Sheria hii na masharti haya kwa kuyatekeleza.+ 20 Hivyo moyo wake hautajikweza juu ya ndugu zake, naye hataacha amri hiyo na kwenda kulia au kushoto, ili aendelee kutawala kwa muda mrefu katika ufalme wake, yeye na wanawe katika Israeli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki