-
Kulinda Utambulisho Wetu wa KikristoMnara wa Mlinzi—2005 | Februari 15
-
-
Biblia inafananisha utambulisho wetu wa Kikristo ulio wazi na mavazi ya nje, yanayovaliwa ili kuonwa na wote. Kuhusu nyakati zetu, Yesu alionya hivi: “Tazama! Ninakuja kama mwizi. Mwenye furaha ni yule anayekaa macho na kutunza mavazi yake ya nje, ili asipate kutembea akiwa uchi na watu waitazame aibu yake.”a (Ufunuo 16:15) Hatungependa kuvua sifa zetu za Kikristo na viwango vya mwenendo na kuruhusu ulimwengu wa Shetani utufinyange. Ikiwa jambo hilo lingetokea, tungepoteza ‘mavazi hayo ya nje.’ Hali hiyo ingekuwa yenye kusikitisha na yenye kuaibisha.
-
-
Kulinda Utambulisho Wetu wa KikristoMnara wa Mlinzi—2005 | Februari 15
-
-
a Huenda maneno hayo yakarejelea kwa njia isiyo ya moja kwa moja kazi za ofisa wa hekalu la mlimani huko Yerusalemu. Wakati wa makesha ya usiku alitembea hekaluni ili kuona ikiwa walinzi Walawi walikuwa macho au walikuwa wamelala mahali pao pa kazi. Mlinzi yeyote aliyepatikana amelala alipigwa kwa kijiti, na huenda mavazi yake ya nje yalichomwa kama adhabu ya kumwaibisha.
-