-
Kuwasiliana na Makao ya RohoAmkeni!—1996 | Novemba 22
-
-
Huyo babaláwo alionyesha ishara kuelekea ubao mkubwa ulioorodhesha mfumo ulio tata wa kuagua ambao watu wake walikuwa wameutumia kwa vizazi visivyohesabika. Ukitegemea kurusha mbegu 16 za mawese, huo ni mfumo ambao umeenea kotekote katika Afrika Magharibi na ng’ambo ya hapo. “Watu hunijia wakiwa na matatizo ya aina zote,” akasema. “Matatizo na wanawake, utasa, ukosefu wa kazi, kurukwa kichwa, afya, na kadhalika. Ikitegemea matokeo ya uaguzi, ombi linafanywa kwa ama wazazi wa kale ama watu wa kimbingu [miungu]. Vyovyote vile, ni lazima aina fulani ya dhabihu itolewe.”
-
-
Kuwasiliana na Makao ya RohoAmkeni!—1996 | Novemba 22
-
-
Ukosefu huo wa uelewevu mara nyingi huhusisha utambulisho wa wale wakaao katika makao ya roho. Kotekote katika Afrika iliyo kusini ya Sahara, kuna itikadi iliyoenea sana kwamba kuna vikundi viwili vya viumbe ambao hukaa katika ulimwengu wa roho. Kikundi cha kwanza ni cha watu wa kimungu, au miungu, ambao hawajapata kuwa binadamu. Cha pili ni cha wazazi wa kale, au roho za wafu, ambao daraka lao ni kuhakikisha kusalimika na ufanisi wa familia zao duniani. Wote miungu na wazazi wa kale inaaminika kuwa wana uwezo wa ama kusaidia ama kudhuru wale walio duniani. Hivyo basi, ni lazima wote waonyeshwe staha na heshima ifaayo.
-