Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Anatutazama kwa Faida Yetu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 15
    • 16. Kazi ya kuhubiri inaonyesha jinsi gani kwamba Yehova anawajali watu walio kama kondoo?

      16 Kazi ya ulimwenguni pote ya kuhubiri ni jambo lingine linaloonyesha kwamba Yehova anawahangaikia watu wenye moyo mnyoofu popote pale wanapoishi. (Mwa. 18:25) Yehova anaweza kuwaongoza watumishi wake kwa watu walio kama kondoo hata ikiwa watu hao wanaishi katika maeneo ambako habari njema hazijahubiriwa, na mara nyingi anatumia malaika ili kufanya hivyo. (Ufu. 14:6, 7) Kwa mfano, kupitia malaika, Mungu alimwongoza Filipo, mweneza-injili wa karne ya kwanza amtafute ofisa Mwethiopia na kumfafanulia Maandiko. Kulikuwa na matokeo gani? Mtu huyo alikubali habari njema na kuwa mfuasi aliyebatizwa wa Yesu.b—Yoh. 10:14; Mdo. 8:26-39.

  • Yehova Anatutazama kwa Faida Yetu
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 15
    • b Mfano mwingine unaoonyesha jinsi Mungu anavyotoa mwongozo unapatikana katika Matendo 16:6-10. Andiko hilo linasema kwamba Paulo na wenzake “walikatazwa na roho takatifu” wasihubiri katika Asia na Bithinia. Badala yake, walitumwa Makedonia, ambako watu wengi wapole waliikubali injili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki