-
Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za YehovaHuduma ya Ufalme—2004 | Februari
-
-
2 Ukiwa Painia-Msaidizi: Je, unaweza kupanga ratiba yako ili utumie muda wa saa 50 katika huduma kwa mwezi mmoja au zaidi katika miezi hii ya utendaji wa pekee? Hutajuta kwa sababu ya marekebisho yoyote utakayofanya katika ratiba yako. (Efe. 5:16) Wengi wameona kwamba kufanya upainia msaidizi huwasaidia waboreshe huduma yao. Wao huwa watulivu zaidi wanapohubiri nao hutumia Biblia zaidi. Kutumia wakati mwingi katika huduma hufanya iwe rahisi kuendelea kuwasaidia watu wowote wanaopendezwa, na wengine ambao hawakuwa na funzo la Biblia walianzisha funzo walipokuwa wakifanya upainia msaidizi. Upainia msaidizi ni utendaji wenye shangwe, kwa sababu tunajitoa kwa ajili ya wengine.—Mdo. 20:35.
3 Usiamue haraka kwamba hali zako hazikuruhusu kufanya upainia msaidizi. Mzee mmoja aliyefanya upainia msaidizi mwaka jana ana watoto wawili na kazi ya wakati wote. Ndugu huyo mwenye shughuli nyingi aliwezaje kutimiza hilo? Kwa kuwa yeye hufanya kazi katikati ya juma, alipanga kuhubiri kwa muda mrefu kwenye miisho-juma, akianza na mahubiri ya barabarani saa moja asubuhi siku za Jumamosi. Wengine katika kutaniko ambao pia walikuwa na hali kama hizo walifanya upainia, nao wakaungana mkono na kutiana moyo. Katika kutaniko lingine, dada mmoja mwenye umri wa miaka 99 aliamua kufanya upainia katika mwezi wa Mei baada ya binti yake kumwomba ajiunge naye. Wengine kutanikoni walimsaidia dada huyo mzee kwenda nyumba kwa nyumba na kwenye mafunzo ya Biblia kwa kusukuma kiti chake cha magurudumu. Pia alihubiri kwa kutumia simu, barabarani, na kuandika barua. Anasadiki kwamba hakufanya hivyo kwa nguvu zake mwenyewe bali tu kwa msaada wa Yehova.—Isa. 40:29-31.
4 Jaribu kutayarisha ratiba inayofaa hali zako. Ratiba zilizo katika toleo hili zinaweza kukusaidia. Je, wewe hufanya kazi wakati wote au huenda shuleni? Huenda ratiba inayohusisha hasa miisho-juma ikakufaa zaidi. Ikiwa una matatizo ya afya na nguvu zako hazikuruhusu kuhubiri kwa saa nyingi, ratiba inayohusisha kuhubiri kwa muda mfupi kila siku huenda ikakufaa zaidi. Ongea na wengine kuhusu tamaa yako ya kufanya upainia msaidizi. Labda wao pia wataweka mradi huo.
5 Njia Ambazo Vijana Wanaweza Kushiriki: Yehova hufurahi vijana wanapotangaza kazi zake za ajabu. (Zab. 71:17; Mt. 21:16) Ikiwa wewe ni kijana na umebatizwa, labda unaweza kufanya upainia msaidizi wakati wa likizo ya shule.
-
-
Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za YehovaHuduma ya Ufalme—2004 | Februari
-
-
8 Jitayarishe Sasa kwa Ajili ya Utendaji Ulioongezeka: Wazee, anzeni sasa kuwachochea wahubiri kutanikoni wawe na hamu ya kufanya upainia msaidizi. Mnaweza kufanya hivyo kwa maelezo yenu yenye kujenga na mfano wenu mwema. (1 Pet. 5:3) Ni wangapi waliofanya upainia msaidizi wakati uliopita? Je, wengi zaidi wanaweza kufanya mwaka huu? Waangalizi wa funzo la kitabu na wasaidizi wao wanapaswa kutafuta njia ya kuwatia wote moyo katika kikundi ili waongeze utendaji wao. Waangalizi wa utumishi wanaweza kupanga mikutano ya ziada ya utumishi wa shambani. Julisheni kutaniko mapema mipango hiyo. Hakikisheni kwamba wahubiri wenye uzoefu wamegawiwa kuongoza na kwamba mikutano ya utumishi inaanza na kumalizika kwa wakati. (Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme, Septemba 2001.) Pia mwangalizi wa utumishi anapaswa kupanga kuwe na eneo, magazeti, na vichapo vya kutosha.
9 Mwaka jana wazee wa kutaniko moja walianza mapema na kwa hamu kuwatia moyo wahubiri wafanye upainia msaidizi, huku baadhi yao wakifanya upainia msaidizi. Walipanga mikutano ya ziada ya utumishi wa shambani—mmoja saa 11:30 alfajiri kwa ajili ya mahubiri ya barabarani, mwingine saa 9 mchana kwa ajili ya wale wanaotoka shuleni, na wa tatu saa 12 jioni kwa ajili ya wale wanaotoka kazini. Zaidi ya hayo, mikutano mitatu ya utumishi wa shambani ilipangwa siku za Jumamosi. Kutaniko liliitikia kwa kuwa na wahubiri 66 waliojiandikisha kuwa mapainia-wasaidizi mwezi wa Aprili!
10 Kwa nini usitenge wakati katika funzo la familia lijalo ili kuweka miradi ya miezi ijayo? Kukiwa na ushirikiano na mipango mizuri, wengine au wote katika familia wanaweza kufanya upainia msaidizi. Ikiwa hilo haliwezekani, wekeni miradi ya kuongeza utendaji wenu kwa kurefusha vipindi vyenu vya kawaida vya kuhubiri au kwa kuhubiri katika pindi za ziada. Salini mkiwa familia kuhusu jambo hilo. Iweni na hakika kwamba Yehova atabariki jitihada zenu.—1 Yoh. 3:22.
-