-
Ushindi wa Kisheria Baada ya Kupambana kwa Muda Mrefu!Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
Hata hivyo, Machi 26, 2004, hakimu alipiga marufuku utendaji mbalimbali wa Mashahidi wa Yehova huko Moscow. Mnamo Juni 16, 2004, Mahakama ya Jiji la Moscow iliunga mkono uamuzi huo.d Akizungumza kuhusu uamuzi huo, Shahidi mmoja wa muda mrefu alisema hivi: “Katika nyakati za Sovieti, Mrusi hakupaswa kuamini kwamba kuna Mungu. Leo, ni lazima Mrusi awe Mwothodoksi.”
Akina ndugu walitenda jinsi gani walipopigwa marufuku? Walitenda kama Nehemia wa kale. Katika siku zake, wakati maadui wa watu wa Mungu walipopinga jitihada zake za kujenga upya ukuta wa Yerusalemu, Nehemia na watu wake hawakujiacha wakengeushwe na upinzani wa aina yoyote. Badala yake, ‘waliendelea kujenga’ na “wakaendelea kuwa na moyo wa kufanya kazi.” (Neh. 4:1-6) Vivyo hivyo, ndugu zetu huko Moscow hawakuacha wapinzani wawakengeushe kutoka katika kazi inayopaswa kufanywa leo, kazi ya kuhubiri habari njema. (1 Pet. 4:12, 16) Walikuwa na uhakika kwamba Yehova angewatunza, na walikuwa tayari kuingia katika hatua ya nne ya mapambano hayo ya muda mrefu.
UPINZANI UNAONGEZEKA
Mnamo Agosti 25, 2004, ndugu zetu walituma ombi lao huko Kremlin ambalo walimwandikia Vladimir Putin, aliyekuwa rais wa Urusi wakati huo. Ombi hilo, ambalo lilieleza jinsi walivyohangaishwa sana na yale marufuku, lilikuwa limeandikwa katika mabuku 76 na lilikuwa limetiwa sahihi zaidi ya 315,000. Wakati huo, viongozi wa kanisa Othodoksi la Urusi walionyesha jinsi walivyo kikweli. Msemaji wa Kiongozi wa Dini wa Moscow alitangaza hivi: “Tunapinga kabisa kazi ya Mashahidi wa Yehova.” Kiongozi mmoja Mwislamu alisema kwamba uamuzi huo wa kupiga marufuku “ulikuwa wa maana sana na wa kihistoria.”
Haishangazi kwamba watu waliopotoshwa katika nchi ya Urusi walipata ujasiri wa kuwashambulia Mashahidi wa Yehova. Mashahidi fulani ambao walikuwa wakishiriki katika kazi ya kuhubiri huko Moscow walipigwa ngumi na mateke na wapinzani. Mwanamume aliyekasirika sana alimkimbiza dada mmoja kutoka katika nyumba fulani na kumpiga teke kwa nguvu sana kwenye uti wa mgongo hivi kwamba dada huyo akaanguka chini kwa kichwa na kuumia. Alihitaji kupata matibabu; lakini polisi hawakumchukulia hatua yoyote mtu aliyemshambulia. Mashahidi wengine walikamatwa na polisi, alama za vidole vyao zikachukuliwa, wakapigwa picha, na kufungwa gerezani usiku kucha. Wasimamizi wa mahali pa kufanyia mikutano huko Moscow walitishwa kwamba wangefutwa kazi ikiwa wangeendelea kuwaruhusu Mashahidi kukodi majengo yao. Muda si muda, makutaniko mengi yalifukuzwa katika majengo waliyokodi. Makutaniko 40 yamelazimika kutumia jengo lenye Majumba manne ya Ufalme. Kutaniko moja linalotumia jengo hilo lililazimika kufanya Mkutano wa Watu Wote saa moja na nusu asubuhi. Mwangalizi mmoja anayesafiri alisema hivi: “Ili kuhudhuria mkutano, wahubiri walihitaji kuamka saa 11 asubuhi, lakini walifanya hivyo kwa kupenda kwa zaidi ya mwaka mmoja.”
“ILI KUWA USHAHIDI”
Ili kuthibitisha kwamba marufuku ya Moscow yalivunja sheria, katika Desemba (Mwezi wa 12) 2004 wanasheria wetu walitafuta msaada katika Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu. (Ona sanduku “Kwa Nini Uamuzi wa Urusi Ulichunguzwa Tena Huko Ufaransa?” kwenye ukurasa wa 6.) Miaka sita baadaye, katika Juni 10, 2010, Mahakama ilifanya uamuzi wa pamoja ambao ulionyesha kwamba Mashahidi wa Yehova hawana hatia hata kidogo!e Mahakama hiyo ilichunguza mashtaka yote ambayo yalitolewa juu yetu na ikapata kwamba hayakuwa na msingi wowote. Ilisema pia kwamba Urusi ilikuwa na daraka la kisheria la “kuzuia uvunjaji wa sheria ambao Mahakama hiyo ilipata na kurekebisha mambo kadiri iwezekanavyo.”—Ona sanduku “Uamuzi wa Mahakama,” kwenye ukurasa wa 8.
-
-
Ushindi wa Kisheria Baada ya Kupambana kwa Muda Mrefu!Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
d Marufuku hayo yalisababisha kufungwa kwa shirika lililoandikishwa kisheria ambalo lilikuwa likitumiwa na makutaniko huko Moscow. Wapinzani walitumaini kwamba kufungwa kwa shirika hilo kungewazuia ndugu zetu kuendelea na huduma yao.
-