Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Betheli ya Brooklyn—Historia ya Miaka 100
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • Betheli ya Brooklyn—Historia ya Miaka 100

      MAMBO muhimu yalitukia katika Jiji la New York mwaka wa 1909. Daraja la Queensboro linalounganisha eneo la Queens na Manhattan lilifunguliwa, na vilevile Daraja la Manhattan linalounganisha eneo la Manhattan na Brooklyn.

      Mambo muhimu pia yalitukia mwaka huo katika utendaji wa Mashahidi wa Yehova. Mapema, Charles Taze Russell, aliyekuwa msimamizi wa shirika la kisheria la Mashahidi wa Yehova (Watch Tower Bible and Tract Society), alikuwa ametambua uwezekano wa kupanua kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Mathayo 24:14) Aliona kwamba kuhamisha makao makuu ya Mashahidi wa Yehova kutoka Pittsburgh, Pennsylvania, hadi Brooklyn, New York, ingekuwa hatua muhimu sana ya kutimiza mradi huo. Matayarisho yalianza mwaka wa 1908, na mapema katika mwaka uliofuata makao makuu yakahamishwa.

      Kwa Nini Makao Makuu Yalihamishiwa Brooklyn?

      Ndugu waliosimamia kazi ya kuhubiri wakati huo walijua kwamba ujumbe wa Biblia uliochapwa katika magazeti ya ulimwengu ulisaidia sana kusambaza kweli za Biblia. Mwaka wa 1908, ujumbe wa Russell kuhusu Biblia ulitokea kila juma katika magazeti 11 ambayo kwa ujumla yalichapisha nakala 402,000.

      Hata hivyo, Russell aliandika: “Ndugu wanaoelewa jinsi makala mbalimbali zinavyosambazwa kati ya magazeti ya ulimwengu . . . wanatuhakikishia kwamba ikiwa yale mahubiri ya kila juma yangeandikwa katika [jiji kubwa] huenda ikawa yangechapishwa kotekote Marekani, na wanakadiria kwamba katika muda wa mwaka mmoja yangekuwa yakichapishwa kwa ukawaida katika mamia ya magazeti.” Kwa hiyo, walianza kutafuta mahali bora kwa ajili ya kupanua kazi ya kuhubiri.

      Kwa nini walichagua Brooklyn? Russell alisema: “Baada ya kusali kuhusu jambo hilo, sote tulikata kauli kwamba eneo la Brooklyn, New York, lenye watu wengi . . . na ambalo linaitwa ‘Mji wa Makanisa,’ linafaa sana kuwa kituo cha kazi ya mavuno.” Matokeo yanaonyesha kwamba uamuzi huo ulikuwa mzuri. Punde si punde, magazeti 2,000 yalikuwa yakichapisha ujumbe wa Biblia wa Russell.

      Jiji la New York lilifaa kwa sababu nyingine pia. Mwaka wa 1909, ofisi za tawi zilikuwa zimefunguliwa nchini Uingereza, Ujerumani, na Australia, na nyingine zingefunguliwa muda mfupi baadaye. Kwa hiyo, lilikuwa jambo la hekima kuwa na makao makuu katika jiji lenye bandari ambalo lilikuwa na mfumo mzuri wa barabara na reli.

      Kwa Nini Makao Makuu Yaliitwa Betheli?

      Makao makuu ya kwanza ya shirika la Watch Tower Bible and Tract Society yalifunguliwa katika miaka ya 1880, huko Allegheny (sasa ni sehemu ya Pittsburgh), Pennsylvania. Wakati huo, makao makuu yaliitwa Nyumba ya Biblia. Katika mwaka wa 1896, watu 12 walikuwa wakifanya kazi huko.

      Makao makuu yalipohamishwa kutoka Allegheny hadi Brooklyn mwaka wa 1909, makao mapya ya wafanyakazi yaliitwa Betheli.a Kwa nini yaliitwa Betheli? Majengo ambayo shirika la Watch Tower Society lilinunua kwenye 13-17 Hicks Street yalikuwa mali ya kasisi mashuhuri aliyeitwa Henry Ward Beecher, nayo yaliitwa Betheli ya Beecher. Makao ya zamani ya Beecher, 124 Columbia Heights, yalinunuliwa pia. Toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 1909 (1/3/1909), lilisema: “Ni jambo la ajabu sana kwamba tulipata Betheli ya Beecher kisha bila kutarajia tukapata makao yake ya zamani. . . . Makao mapya yataitwa ‘Betheli,’ na ukumbi na ofisi mpya itaitwa ‘Maskani ya Brooklyn.’ Majina haya yatatumiwa badala ya jina ‘Nyumba ya Biblia.’”

  • Betheli ya Brooklyn—Historia ya Miaka 100
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • Wageni Wakaribishwa kwa Uchangamfu

      Majengo hayo yaliwekwa wakfu Januari 31, 1909 (31/1/1909). Jumatatu (Siku ya 1), Septemba 6, 1909 (6/9/1909), ilikuwa siku ya wageni huko Betheli. Mamia ya Wanafunzi wa Biblia, kama Mashahidi wa Yehova walivyoitwa wakati huo, walitembelea Betheli siku hiyo. Wengi wao walikuwa wamehudhuria kusanyiko la Kikristo huko Saratoga Springs, umbali wa kilomita 320 hivi kaskazini ya Jiji la New York. Ndugu Charles Taze Russell mwenyewe aliwakaribisha wageni hao.b

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki