-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Jiji la Sarajevo lilipozingirwa, Ljiljana Ninković na mume wake Nenad walinaswa jijini na kutenganishwa na binti zao wawili. Ljiljana anasema: “Tulikuwa familia ya kawaida yenye watoto wawili, nasi tulikuwa na nyumba na gari. Halafu kwa ghafula, mambo yakabadilika kabisa.”
Lakini mara nyingi waliona mkono wa Yehova ukiwalinda. Ljiljana anaendelea kusimulia: “Nyumba yetu ililipuliwa kwa bomu mara mbili baada tu ya sisi kuondoka. Ingawa tulipata matatizo, tulifurahia mambo madogo-madogo. Kwa mfano, tulifurahia kwenda kwenye bustani kuchuna majani fulani (ya dandelion) ili kutengeneza saladi, hivyo hatukula wali mkavu. Tulijifunza kutosheka na vitu tulivyokuwa navyo na kutochezea kitu chochote.”
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 197]
Ljiljana akiwa na binti zake
-