-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Veronika Babić alizaliwa huko Kroatia, na familia yake ilianza kujifunza Biblia katikati ya miaka ya 1950. Baada ya kubatizwa mwaka wa 1957, Veronika alihamia Sarajevo, Bosnia, pamoja na mume wake. Milica Radišić, ambaye alitoka katika eneo la Slavonia, huko Kroatia, alibatizwa mwaka wa 1950. Familia yake pia ilihamia Bosnia. Zikishirikiana, familia hizo zilianza kueneza kweli ya Ufalme huko Bosnia. Kama katika sehemu nyingine za Yugoslavia, walipaswa kuhubiri kwa uangalifu. Veronika anaeleza: “Tulishtakiwa kwa polisi, na vichapo vyetu vikachukuliwa. Tulikamatwa, tukahojiwa, tukatishwa kwamba tutatiwa gerezani, na tukatozwa faini. Hata hivyo, hakuna jambo lolote lililoweza kutuvunja moyo au kutuogopesha. Badala yake, yote hayo yaliimarisha imani yetu katika Yehova.”
Milica anakumbuka: “Siku moja, mwanamume mmoja alikuja kwenye Jumba la Ufalme na akaonyesha kupendezwa na Biblia. Alikaribishwa vizuri na hata akakaa kwa muda katika nyumba za akina ndugu. Alitoa maelezo kwa bidii kwenye mikutano. Lakini baadaye binti yetu, akiwa mahali pake pa kazi, alimwona mwanamume huyo akihudhuria mkutano wa polisi wa siri. Kisha, tukatambua kwamba alikuwa ametumwa na polisi ili kutupeleleza. Kwa kuwa uhusiano wake na polisi haukuwa tena jambo la siri, aliacha kuja.”
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Katika mwaka wa 1963, waligeuza kibanda kimoja cha kurekebishia magari huko Sarajevo kuwa jumba, ambalo lilitumiwa na kutaniko la kwanza huko Bosnia na Herzegovina.
-