Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • 13. Ni nini kinachofananishwa na (a) mzeituni, (b) mzizi wake, (c) shina lake, na (d) matawi yake?

      13 Mtume Paulo anawalinganisha wale ambao wanakuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu na matawi ya mzeituni wa mfano.a (Rom. 11:21)

  • ‘Lo! Jinsi Kilivyo Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Mei 15
    • Matawi yote hayo kwa pamoja yanafananisha “hesabu kamili” ya wale ambao wanatiwa ndani ya sehemu ya pili ya uzao wa Abrahamu.

      14, 15. Ni nani ‘waliokatwa’ kutoka kwenye mzeituni uliopandwa, na ni nani waliopandikizwa kwenye mzeituni huo?

      14 Katika mfano wa mzeituni, Wayahudi wa asili ambao walimkataa Yesu wanalinganishwa na matawi ambayo “yalikatwa.” (Rom. 11:17) Hivyo, walipoteza nafasi ya kuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu. Lakini ni nani ambao wangechukua mahali pao? Wayahudi wa asili ambao walijivunia kuwa wazao wa kimwili wa Abrahamu hawakufikiri kamwe kwamba watu wengine wangeweza kuchukua mahali pao. Lakini Yohana Mbatizaji alikuwa tayari amewaonya kwamba ikiwa Yehova angetaka, angeweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka katika mawe.—Luka 3:8.

      15 Basi, Yehova alifanya nini ili kutimiza kusudi lake? Paulo anaeleza kwamba matawi kutoka kwenye mzeituni wa mwituni yalipandikizwa kwenye mzeituni uliopandwa ili kuchukua mahali pa yale matawi yaliyokatwa. (Soma Waroma 11:17, 18.) Hivyo, Wakristo watiwa-mafuta wa mataifa, kama Wakristo fulani katika kutaniko la Roma, walipandikizwa kwa njia ya mfano kwenye mzeituni huo wa mfano. Katika njia hiyo walikuja kuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu. Mwanzoni, walikuwa kama matawi ya mzeituni wa mwituni, kwa sababu hawakuwa na nafasi yoyote ya kuwa sehemu ya agano hilo la pekee. Lakini Yehova aliwafungulia njia ili wawe Wayahudi wa kiroho.—Rom. 2:28, 29.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki