-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
MAJENGO MAPYA YA OFISI YA TAWI NA MAJUMBA YA UFALME
Sawa na inavyokuwa katika sehemu nyingine, familia ya Betheli huko Zagreb, Kroatia, ilianza kujionea matokeo ya ukuzi wa kiroho. Idadi ya familia ya Betheli iliongezeka kutoka watu 10 mpaka karibu 50. Lakini kwa kuwa Makao ya Betheli yalikusudiwa wenzi wa ndoa wanne au watano tu, ilibidi nyumba nyingine zilizo karibu zikodiwe.
Muda mfupi baada ya Halmashauri ya Tawi kuundwa, Baraza Linaloongoza liliagiza halmashauri hiyo inunue uwanja huko Zagreb kwa ajili ya ujenzi wa Makao mapya ya Betheli. Baada ya muda mfupi, wajitoleaji wenyeji na watumishi wa kimataifa walijenga majengo maridadi ambayo yangesaidia kuendeleza mambo ya Ufalme kwa miaka mingi. Majengo hayo mapya ya ofisi ya tawi na Jumba la Ufalme yaliwekwa wakfu Jumamosi, Oktoba 23, 1999, kutia ndani jengo lenye Majumba mawili ya Ufalme ambalo liko katikati ya Zagreb. Wajumbe kutoka nchi 15 walihudhuria, kutia ndani Ndugu Gerrit Lösch wa Baraza Linaloongoza, ambaye alitoa hotuba ya wakfu. Siku iliyofuata, watu 4,886 walikusanyika kwa ajili ya programu ya kiroho yenye kufurahisha katika ukumbi mkubwa wa michezo. Hiyo ilikuwa siku isiyoweza kusahaulika kwa watu wa Yehova nchini Kroatia—na wengi wao walikuwa wamemtumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka 50 au zaidi huku wakivumilia hali zenye kuogopesha sana katika historia ya kisasa!
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 216]
Halmashauri ya Tawi ya Kroatia, na ofisi ya tawi
-