-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Jumamosi, Mei 29, 2010, kwenye ofisi ya tawi ya Papua New Guinea, akina ndugu na dada 500 hivi kutoka nchi 12 walikusanyika kusikia hotuba ya kuwekwa wakfu ikitolewa na Winston Payne, wa ofisi ya tawi ya Australia. Majengo yaliyopanuliwa ya ofisi hiyo yalitia ndani jengo la orofa nne lenye vyumba vya kulala, chumba cha kulia chakula, jikoni, na dobi; jengo la huduma nyingine lililo na Jumba la Ufalme; na ofisi ya tafsiri yenye nafasi kubwa sana. Wasikilizaji walitia ndani kikundi cha Mashahidi waliokuwa wametembea kwa siku sita kupitia milima yenye miamba ili kuhudhuria tukio hilo. Kikundi hicho kilikuwa kimevalia mavazi ya kitamaduni ya Orokaiva na waliwakaribisha wageni wengine kwa uchangamfu wakicheza dansi na kuimba. Akiwa na machozi, dada mmoja ambaye alibatizwa miaka mingi iliyopita alieleza hisia ambazo zilifanana na za watu wengi aliposema, “Leo ninahisi ni kana kwamba tayari niko katika Paradiso!”
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 37]
Winston Payne alitoa hotuba ya kuwekwa wakfu ya ofisi ya tawi ya Papua New Guinea
-