-
Rumania2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwa kuwa habari njema ilikuwa ikienea sana, Jacob B. Sima, Mwanafunzi wa Biblia mwenye asili ya Kirumania, alitumwa Rumania kusaidia kupanga kazi ya kuhubiri na kuiandikisha kisheria. Punde baada ya kufika Cluj-Napoca mnamo mwaka wa 1920, Ndugu Sima alifanya mkutano na Károly Szabó, na baadaye József Kiss. Hangaiko lao kuu lilikuwa kupata nyumba inayofaa jijini Cluj-Napoca ambayo ingetumiwa kama ofisi ya tawi. Hata hivyo, kwa sababu ya upungufu wa nyumba, ndugu hao waliamua kufungua ofisi nyumbani kwa ndugu fulani. Kwa hiyo, ofisi ya tawi ya kwanza ilifunguliwa Aprili 1920 na shirika la kisheria la Mashahidi wa Yehova likaandikishwa. Ofisi ya tawi ya Rumania ilisimamia kazi kwa muda pia katika nchi ya Albania, Bulgaria, Hungaria, na ile iliyokuwa Yugoslavia.
-
-
Rumania2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 77]
Ujenzi wa ofisi mpya jijini Cluj-Napoca, mwaka wa 1924
-