Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
    • “Amri Zake Si Zenye Kulemea”

      4-6. (a) Ni nini maana halisi ya neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘-enye kulemea’? (b) Kwa nini twaweza kusema kwamba amri za Mungu si zenye kulemea?

      4 “Uzishike amri zake.” Kwa msingi, hilo ndilo Mungu atazamia tufanye. Je, anaomba mengi mno? La hasha. Mtume Yohana atuambia jambo fulani lenye kutia moyo sana juu ya amri, au matakwa, ya Mungu. Aliandika hivi: “Hivi ndivyo kumpenda Mungu humaanisha, kwamba tushike amri zake; na bado amri zake si zenye kulemea.”—1 Yohana 5:3.

      5 Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘-enye kulemea’ lamaanisha kihalisi “-zito.” Laweza kurejezea jambo lililo gumu kuishi kulingana nalo au lililo gumu kufuata. Kwenye Mathayo 23:4, neno lilo hilo linatumiwa kufafanua ile “mizigo mizito,” yaani amri na mapokeo ya kufanywa na wanadamu, ambayo waandishi na Mafarisayo waliwekea watu. Je, unapata maana ya mkataa unaofikiwa na mtume Yohana mwenye umri mkubwa? Amri za Mungu si mzigo mzito wenye kulemea, wala si ngumu sana tusiweze kuzitimiza. (Linganisha Kumbukumbu la Torati 30:11.) Kinyume cha hilo, tunapompenda Mungu, kutimiza matakwa yake hutufurahisha. Hutupa sisi fursa yenye thamani ya kuonyesha kumpenda kwetu Yehova.

  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
    • 12. Ungeelezaje ni kwa nini kuendelea kutwaa ujuzi juu ya Mungu na makusudi yake si mzigo wenye kulemea?

      12 Je, kuendelea kutwaa ujuzi huo juu ya Mungu na makusudi yake ni mzigo wenye kulemea? La hasha! Je, waweza kukumbuka jinsi ulivyohisi ulipojifunza kwa mara ya kwanza kwamba jina la Mungu ni Yehova, kwamba Ufalme wake utarudisha Paradiso kwenye dunia hii, kwamba alimtoa Mwana wake mpendwa awe fidia kwa ajili ya dhambi zetu, pamoja na kweli nyinginezo zenye thamani? Je, hilo halikuwa kama kuondoa shela ya ukosefu wa ujuzi na kuona mambo kwa wazi kwa mara ya kwanza? Kuendelea kutwaa ujuzi juu ya Mungu si mzigo wenye kulemea. Ni jambo lenye kupendeza!—Zaburi 1:1-3; 119:97.

  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
    • 16. Eleza ni kwa nini kufikia viwango vya Mungu vya mwenendo sawa na kukubali kweli yake si mzigo wenye kulemea.

      16 Je, kufikia kwetu viwango vya Mungu vya mwenendo sawa na kukubali kweli yake ni mzigo wenye kulemea? Sivyo tunapofikiria manufaa—ndoa ambazo katika hizo mume na mke wanapendana na wana itibari katika mmoja na mwenzake badala ya ndoa ambazo zimevunjika kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu; makao ambako watoto huhisi wanapendwa na wanatakwa na wazazi wao badala ya familia ambazo katika hizo watoto wanahisi hawapendwi, wanapuuzwa, na hawatakwi; dhamiri safi na afya njema badala ya hisia za kuwa na hatia na mwili uliokumbwa na UKIMWI au maradhi mengine ya kupitishwa kingono. Kwa hakika, matakwa ya Yehova hayatunyimi chochote kile tunachohitaji ili kufurahia uhai!—Kumbukumbu la Torati 10:12, 13.

  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
    • 19. Eleza jinsi tunavyonufaika kutokana na kustahi uhai na damu.

      19 Je, kuona kwetu uhai na damu kuwa takatifu ni mzigo wenye kulemea? La, hasha! Ebu fikiria. Je, uhuru pasipo kansa ya mapafu inayosababishwa na kuvuta tumbaku ni mzigo wenye kulemea? Je, kuponyoka uraibu wa kiakili na wa kimwili wa madawa yenye kudhuru ni mzigo wenye kulemea? Je, kuepuka kupatwa na UKIMWI, mchochota wa ini, au maradhi mengine yanayotokana na utiaji-damu mishipani ni mzigo wenye kulemea? Kwa wazi, kujiepusha kwetu na tabia na mazoea yenye kudhuru ni kwa faida yetu.—Isaya 48:17.

      20. Familia moja ilinufaikaje kutokana na kuwa na maoni ya Mungu juu ya uhai?

      20 Fikiria ono hili. Miaka kadhaa iliyopita, mwanamke Shahidi aliyekuwa na mimba ya karibu miezi mitatu na nusu alianza kutokwa na damu jioni moja naye akapelekwa hospitali mbio. Baada ya daktari kumchunguza, mwanamke huyo alimsikia akimwambia mmoja wa wauguzi kwamba wangelazimika kuikomesha mimba hiyo. Akijua maoni ya Yehova juu ya uhai wa watoto wasiozaliwa bado, yeye alikataa katakata utoaji-mimba akimwambia daktari hivi: “Ikiwa yu hai, mwache humo!” Aliendelea kutokwa na damu mara kwa mara, lakini miezi kadhaa baadaye alizaa kabla ya wakati wake, kitoto kivulana chenye afya, ambaye sasa ni mwenye umri wa miaka 17. Alieleza hivi: “Mwana wetu aliambiwa haya yote, naye alisema anaterema kwamba hakutupwa. Ajua kwamba sababu tu ya yeye hata kuwa hai ni kumtumikia kwetu Yehova.” Kwa hakika, kuwa na maoni ya Mungu juu ya uhai hakukuwa mzigo wenye kulemea kwa familia hii!

  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
    • 23, 24. Twaweza kuonyesha kwa kielezi gani kwamba kumtumikia Yehova pamoja na watu wake waliofanywa kuwa tengenezo si mzigo wenye kulemea?

      23 Je, kumtumikia Yehova pamoja na watu wake waliofanywa kuwa tengenezo ni mzigo wenye kulemea? La hasha! Kinyume cha hilo, ni pendeleo lenye thamani kuwa na upendo na utegemezo wa familia ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada Wakristo! (1 Petro 2:17) Ebu wazia umeokoka mvunjiko wa meli na wajipata majini, uking’ang’ana kuelea. Unapohisi kwamba huwezi kuvumilia zaidi, mkono wakufikilia kutoka katika mashua ya kuokolea uhai. Ndiyo, kuna waokokaji wengine! Katika mashua hiyo ya kuokolea uhai, wewe na wengine mnapiga makasia kwa zamu hadi pwani mkiwachukua waokokaji wengine njiani.

  • Kusaidia Wengine Wajifunze Matakwa ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
    • Jambo Gumu Lakini Si Mzigo Wenye Kulemea

      4. Ni kielezi gani kiwezacho kutumiwa ili kuonyesha kwamba wajibu wetu wa kuhubiri habari njema si mzigo wenye kulemea?

      4 Je, kuhubiri habari njema hii ni mzigo wenye kulemea? Sivyo hata kidogo! Kwa kutoa kielezi: Baba ana wajibu wa kuiandalia familia yake kimwili. Akishindwa kufanya hivyo ni kama ameikana imani ya Kikristo. Mtume Paulo aliandika hivi: “Hakika ikiwa yeyote hawaandalii kitu wale walio wake mwenyewe, na hasa kwa ajili ya wale walio washiriki wa nyumbani mwake, ameikana imani naye ni mbaya zaidi kuliko mtu asiye na imani.” (1 Timotheo 5:8) Lakini je, wajibu huo ni mzigo wenye kulemea kwa mwanamume Mkristo? Sivyo ikiwa anaipenda familia yake, kwa maana ikiwa aipenda yeye ataka kuiandalia.

      5. Ingawa kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi ni wajibu, kwa nini twapaswa kufurahia kuifanya?

      5 Vivyo hivyo, kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi ni wajibu, ni takwa, ambao uhai wetu wenyewe wategemea. Paulo alieleza hivi: “Nimewekewa sharti. Kwa kweli, ole wangu mimi ikiwa sikutangaza habari njema!” (1 Wakorintho 9:16; linganisha Ezekieli 33:7-9.) Hata hivyo, nia yetu ya kuhubiri ni upendo, si wajibu tu. Kwanza kabisa twampenda Mungu, lakini pia twawapenda majirani wetu, na twajua jinsi lilivyo jambo la maana kwao kuisikia habari njema. (Mathayo 22:37-39) Inawapa tumaini la wakati ujao. Karibuni Ufalme wa Mungu utasahihisha udhalimu mbalimbali, utaondoa uonevu wote, na kurudisha amani na muungano—yote kwa baraka idumuyo milele ya wale wanaojitiisha chini ya utawala wao mwadilifu. Je, hatufurahi, ndiyo kusisimka, kushiriki na wengine habari njema hiyo?—Zaburi 110:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki