-
Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
13. Ni kwa njia gani tunaweza kuendelea kuwa wanyoofu tunapokuwa na uhusiano wa kikazi pamoja na mwamini mwenzetu?
13 Tunashughulika kwa unyoofu na waamini wenzetu katika mambo ya kibiashara pia. Nyakati nyingine, huenda akina ndugu na dada Wakristo wakashirikiana kufanya biashara. Wanapaswa kuwa waangalifu wasichanganye mambo hayo na ibada yao katika Jumba la Ufalme au katika huduma. Huenda uhusiano wao wa kikazi ukawa ule wa tajiri na mfanyakazi. Tukiwaajiri akina ndugu au dada, tuhakikishe kwamba tunawatendea kwa unyoofu, tunawalipa kwa wakati, tunawalipa mshahara ambao tumekubaliana, na kuwatimizia mambo mengine ambayo wafanyakazi wanastahili kulingana na sheria za nchi. (1 Timotheo 5:18; Yakobo 5:1-4) Kwa upande mwingine, ikiwa tumeajiriwa na ndugu au dada, tutafanya kikamili kazi tunayolipwa kufanya. (2 Wathesalonike 3:10) Hatutazamii kutendewa kwa njia ya pekee eti kwa sababu ya uhusiano wetu wa kiroho, kana kwamba tajiri wetu anawajibika kutupa likizo au marupurupu mengine ambayo wafanyakazi wengine hawapewi.—Waefeso 6:5-8.
-
-
Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
UNYOOFU KATIKA SHUGHULI ZA KIMWILI
15. Yehova ana maoni gani kuhusu mazoea ya kibiashara yenye udanganyifu, na Wakristo wanapaswa kuwa na maoni gani kuhusu mazoea hayo yaliyoenea sana?
15 Mkristo anapaswa kuwa mnyoofu hata nje ya kutaniko. Paulo alisema: “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.” (Waebrania 13:18) Muumba wetu anatazamia tuwe wanyoofu katika shughuli za kibiashara. Katika kitabu cha Methali peke yake, mizani ya udanganyifu inazungumziwa katika mistari minne. (Methali 11:1; 16:11; 20:10, 23) Zamani za kale, kwa kawaida watu walitumia mizani na mawe ya mizani katika shughuli za kibiashara ili kupima uzito wa bidhaa zilizonunuliwa na pesa zilizotumiwa kuzilipia. Wanabiashara wasio wanyoofu walitumia mizani yenye kasoro na aina mbili za mawe ya mizani ili kuwadanganya na kuwaibia wateja wao.c Yehova anachukia matendo kama hayo! Ili kukaa katika upendo wake, tunapaswa kuepuka kabisa mazoea yote ya kibiashara yenye udanganyifu.
-
-
Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
c Walitumia aina moja ya mawe ya mizani waliponunua vitu na ile nyingine walipouza vitu, na katika visa vyote viwili walijifaidi wenyewe tu. Pia, nyakati nyingine walitumia mizani ambayo upande wake mmoja ulikuwa mrefu zaidi au mzito zaidi ya ule mwingine ili kumdanganya mteja wakati wowote ule.
-