Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Biblia Katika Lugha ya Maisha ya Kila Siku
    Amkeni!—1997 | Aprili 8
    • Tafsiri Inayotakasa Jina la Mungu

      Kwenye Mathayo 6:9, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kusali hivi: “Baba yetu uliye katika mbingu, jina lako na litakaswe.” Hata hivyo, katika tafsiri zilizo nyingi, Mungu ni mtu asiye na jina, atambulishwaye tu kwa jina la cheo “Mungu” au “Bwana.” Hata hivyo hali haikuwa hivyo mwanzoni. Mungu alitambulishwa kwa wazi karibu mara 7,000 katika Maandiko ya Kiebrania ya awali kwa jina la kibinafsi “Yehova.” (Kutoka 3:15; Zaburi 83:18) Katika miaka ya baadaye hofu za kishirikina ziliwafanya Wayahudi wakome kulitumia jina la kimungu. Baada ya kifo cha mitume wa Yesu, maoni hayo ya kishirikina yaliathiri kutaniko la Kikristo. (Linganisha Matendo 20:29, 30; 1 Timotheo 4:1.) Wenye kunakili sehemu za Kigiriki za Maandiko walianza kuweka mahali pa jina la kibinafsi la Mungu, Yehova, maneno ya Kigiriki Kyʹri·os na The·osʹ, yanayomaanisha “Bwana” na “Mungu.”

      Kwa furaha, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya imechukua ile hatua yenye ujasiri ya kurudisha jina Yehova kwenye Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (“Agano Jipya”), jina hilo linaonekana mara 237. Kurudisha huko hakutegemei vile watafsiri watakavyo, bali wategemea usomi timamu, wenye uangalifu. Kwa kielelezo, Luka 4:18 hunukuu maneno ya Isaya 61:1. Katika maandishi ya Kiebrania ya awali, jina Yehova lilionekana katika mstari huo wa Isaya.b Kwa kufaa basi, katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, Luka 4:18 limetafsiriwa hivi: “Roho ya Yehova iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kutangaza habari njema kwa walio maskini.”

      Fasiri hizo husaidia pia wasomaji watofautishe Yehova Mungu na Mwana wake mzaliwa-pekee, Yesu Kristo. Mathalani, tafsiri zilizo nyingi hufasiri Mathayo 22:44 hivi: “Bwana alimwambia Bwana wangu.” Lakini ni nani asemaye na anasema na nani? Kwa kweli, mstari huo ni nukuu kutoka Zaburi 110:1, ambalo, katika maandishi ya Kiebrania ya awali, lina jina la kimungu. Kwa hiyo Tafsiri ya Ulimwengu Mpya hufasiri mstari huo hivi: “Yehova alimwambia Bwana wangu: ‘Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwekapo maadui wako chini ya miguu yako.’” Kufahamu ile tofauti ambayo Maandiko huonyesha kati ya Yehova Mungu na Mwana wake si jambo la kitaalamu. (Marko 13:32; Yohana 8:17, 18; 14:28) Ni jambo la maana kwa habari ya wokovu wa mtu. Lasema Matendo 2:21: “Kila mtu aitiaye jina la Yehova ataokolewa.”

  • Biblia Katika Lugha ya Maisha ya Kila Siku
    Amkeni!—1997 | Aprili 8
    • b Ni kweli kwamba tafsiri ya Septuagint ya Kigiriki ilikuwa msingi wa manukuu ya Maandiko ya Kiebrania katika lile lenye kuitwa isivyofaa, Agano Jipya. Kwa kuwa nakala za baadaye za Septuagint hazina jina la kimungu, wasomi wengi hujadili kwamba jina hilo halipaswi vilevile kutiwa ndani katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Hata hivyo, nakala zilizoko za zamani zaidi za Septuagint zina hilo jina Yehova—katika namna yalo ya Kiebrania cha awali. Hilo lategemeza kwa nguvu kule kurudishwa kwa jina Yehova katika Maandiko ya Kigiriki.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki