-
“Fulizeni Kulinda”Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 15
-
-
Kutoa Kielezi cha Uhitaji wa Kulinda
9, 10. (a) Ungeelezaje kwa kifupi kielezi cha Yesu cha watumwa ambao walimngojea bwana-mkubwa wao arudi kutoka kufunga ndoa? (b) Kwa nini huenda ilikuwa vigumu kwa watumwa kumngojea bwana-mkubwa wao? (c) Kwa nini lilikuwa jambo lenye manufaa kwa watumwa hao kuwa wenye saburi?
9 Akikazia uhitaji wa kulinda, Yesu aliwalinganisha wanafunzi wake na watumwa wanaomngojea bwana-mkubwa wao arudi kutoka kufunga ndoa. Walijua kwamba atarudi usiku fulani—lakini saa ngapi? Je, ni katika lindo la kwanza la usiku? La pili? La tatu? Hawakujua. Yesu alisema: “Ikiwa [bwana-mkubwa] awasili katika lindo la pili, hata ikiwa ni katika la tatu, na awakuta hivyo [wakilinda], wenye furaha ni wao!” (Luka 12:35-38) Ebu wazia msisimko wa watumwa hao. Hakika kila sauti, kila kivuli chenye kupita kingeongeza taraja lao: ‘Je, huyo ndiye bwana-mkubwa wetu?’
10 Ingekuwaje kama bwana-mkubwa angewasili wakati wa lindo la pili la usiku, ambalo lilikuwa kati ya saa tatu usiku hadi katikati ya usiku? Je, watumwa wote, hata wale waliokuwa wamefanya kazi kwa bidii tangu asubuhi na mapema, wangekuwa tayari kumlaki, au wengine kati yao wangekuwa wamelala usingizi? Vipi ikiwa bwana-mkubwa angerudi wakati wa lindo la tatu la usiku—kile kipindi cha kati ya katikati ya usiku hadi karibu saa tisa usiku? Je, watumwa wengine wangevunjika moyo, au hata kukerwa na kule walikodhania kuwa kukawia?a Ni wale tu waliopatikana wakilinda wakati ambapo bwana-mkubwa alifika ndio wangetangazwa kuwa wenye furaha. Kwa hakika, maneno haya ya Mithali 13:12 yangewahusu: “Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.”
-
-
“Fulizeni Kulinda”Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 15
-
-
a Bwana-mkubwa hakuwa amefanya miadi yoyote na watumwa wake. Basi, hakuwa na wajibu wowote wa kuwajulisha watumwa utendaji wake, wala kuwaeleza sababu ya kule kulikoonekana kuwa kukawia kwake.
-