Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Konstantino Mkubwa Je, Alikuwa Mtetezi wa Ukristo?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Machi 15
    • Mwaka wa 313 W.K., Konstantino alipanga kushirikiana na Maliki Lisinio, mtawala wa majimbo ya mashariki. Kupitia ile Amri ya Milan, kwa pamoja walitoa uhuru wa kuabudu na haki sawa kwa vikundi vyote vya kidini. Hata hivyo, wanahistoria wengi hupunguza umaana wa hati hiyo, wakisema kwamba ilikuwa barua ya kawaida tu wala si hati kuu ya kimaliki yenye kuonyesha badiliko la sera kuelekea Ukristo.

  • Konstantino Mkubwa Je, Alikuwa Mtetezi wa Ukristo?
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Machi 15
    • Dini Katika Mkakati wa Konstantino

      Kuhusu mtazamo wa ujumla ambao maliki wa Roma wa karne ya tatu na ya nne walikuwa nao kuelekea dini, kitabu Istoria tou Ellinikou Ethnous (Historia ya Taifa la Kigiriki) chasema hivi: “Hata wakati ambapo wale waliokalia kiti cha ufalme cha hiyo milki hawakuwa na mielekeo ya kidini yenye kina sana, wakikubaliana na kufikiri kwa nyakati hizo, waliliona kuwa jambo la lazima kuitanguliza dini katika muundo wao wa mipango ya kisiasa, ili angalau kuyapa matendo yao sifa ya kidini.”

      Bila shaka, Konstantino alikuwa mtu aliyepatanisha maisha yake na nyakati ambamo aliishi. Mwanzoni mwa kazi-maisha yake, alihitaji tegemezo fulani la “kimungu,” na hilo halingeweza kuandaliwa na miungu ya Roma iliyokuwa ikififia. Hiyo milki kutia na dini yake na mashirika mengine, ilikuwa ikishuka, na jambo fulani jipya na lenye kutia nguvu lilihitajiwa ili kuiimarisha tena. Ensaiklopedia Hidria yasema hivi: “Konstantino hasa alipendezwa na Ukristo kwa sababu haukutegemeza tu ushindi wake bali pia kule kutengeneza upya milki yake. Makanisa ya Kikristo yaliyokuwako kila mahali yakawa tegemezo lake la kisiasa. . . . Alijiweka karibu na maaskofu wakubwa wa hizo nyakati . . . , akaomba kwamba watunze muungano wao ukiwa kamili.”

      Konstantino alihisi kwamba dini ya “Kikristo”—hata ingawa ilikuwa yenye kuasi na kufisidiwa sana kufikia wakati huo—ingeweza kutumiwa kwa matokeo ikiwa kani yenye kutia nguvu mpya na yenye kuunganisha ili kuusaidia mpango wake mkubwa wa utawala wa kimaliki. Akikubali kirasmi misingi ya Ukristo wenye kuasi imani ili kupata tegemezo katika kuendeleza malengo yake mwenyewe ya kisiasa, aliamua kuunganisha watu chini ya “katoliki,” au dini ya watu wote. Desturi na sherehe za kipagani zilipewa majina ya “Kikristo.” Na makasisi wa “Kikristo” wakapewa hadhi, mshahara, na uwezo wenye kuvutia sawa na makasisi wa kipagani.

      Akitafuta upatano wa kidini kwa sababu za kisiasa, upesi Konstantino alinyamazisha kabisa hoja zenye kupinga, sio kwa msingi wa kweli ya mafundisho, bali kwa msingi wa kibali cha walio wengi. Tofauti kubwa sana za kimafundisho ndani ya kanisa la “Kikristo” lililokuwa limegawanyika vibaya, zilimpa fursa ya kuingilia kati akiwa mpatanishi “mwenye kutumwa na Mungu.” Kupitia shughuli zake na Wadonati katika Afrika Kaskazini na wafuasi wa Ariasi katika sehemu ya mashariki ya hiyo milki, aligundua upesi kwamba kushawishi hakukutosha kufanyiza imani thabiti, yenye kuungamanishwa.a Ilikuwa ni kwa kujaribu kutatua ule ubishi wa Kiaria kwamba alifanya mkutano wa baraza la kwanza la muungano wa kidini katika historia ya kanisa.—Ona sanduku “Konstantino na Baraza la Nisea.”

      Kumhusu Konstantino, mwanahistoria Paul Johnson ataarifu hivi: “Huenda mojawapo ya sababu zake kuu za kuuvumilia Ukristo ikawa kwamba ulimpa yeye mwenyewe na Serikali fursa ya kudhibiti kabisa sera ya Kanisa juu ya mafundisho.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki