-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
WATU WA FAMILIA WALIPENDEZWA. Alejandro, ndugu anayeishi Kolombia, alitaka kuwahubiria watu wa familia yao. Kwa sababu wanaishi mbali, aliwaandikia barua na kuwatumia nakala kadhaa za magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Pablo, mtu wa familia yao, aliposoma magazeti na maandiko yaliyomo, alitambua kwamba mafundisho ya Kanisa Katoliki ni ya uwongo. Akiwa na furaha nyingi, aliwaeleza watu wengine wa familia mambo aliyojifunza nao pia wakatambua kwamba ni ya kweli, na hivyo wakaacha kushirikiana na Kanisa Katoliki.
Muda si muda, watu 15 wa familia hiyo wakaanza kukutana kila usiku ili kujifunza Biblia wakitumia magazeti hayo. Kwa kuwa walitaka kujua zaidi, walitafuta Mashahidi katika miji iliyo karibu lakini hawakuwapata. Wakati huohuo, walianza kuwaeleza majirani wao mambo waliyokuwa wamejifunza. Hatimaye, wakatambua kwamba kuna Jumba la Ufalme katika mji uliokuwa umbali wa kilomita 80 hivi. Mara moja wakaenda huko na kuwaomba ndugu wawasaidie kujua mengi kuhusu Biblia.
Sasa painia wa kawaida huenda huko mara moja kwa juma ili kuongoza funzo moja la Biblia lenye watu 26, yaani, familia ya Alejandro na watu wengine 11. Wao hukodi gari ili wengi wao waweze kuhudhuria hotuba ya watu wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi.
-
-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 64]
Samaniego, Nariño, Kolombia
-