-
Yehova Amekuwa Kimbilio LanguMnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
-
-
Upesi Dimitris akapewa mgawo wa kufundisha kwenye shule katika Vathy, mji mkuu wa kisiwa hicho. Aliendelea kusoma fasihi za Wanafunzi wa Biblia, na usiku mmoja wenye mvua nyingi wawili kati yao kutoka kisiwa cha Chios walituzuru. Walikuwa wamerudi kutoka Marekani ili kutumikia wakiwa makolpota, kama vile waeneza-evanjeli wa wakati wote walivyokuwa wakiitwa wakati huo. Tuliwapa makao usiku huo, nao wakatuambia mambo mengi kuhusu makusudi ya Mungu.
-
-
Yehova Amekuwa Kimbilio LanguMnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
-
-
Karibu na wakati huo tulipata kujua kwamba Mwanafunzi mwingine wa Biblia—aliyekuwa kolpota pia—alikuwa amekuja Samos. Tuliposikia kwamba polisi walikuwa wamekataa kumpa ruhusa ya kutoa hotuba ya Biblia ya watu wote, tulienda kumtafuta. Tulimpata katika duka akizungumza na wanatheolojia wawili wa Othodoksi ya Kigiriki. Wakiona aibu kwa sababu ya kutoweza kutetea itikadi zao kwa kutumia Biblia, hao wanatheolojia waliondoka upesi. Mume wangu, akiwa amevutiwa na ujuzi wa huyo kolpota, akauliza: “Ni vipi kwamba waweza kuitumia Biblia kwa urahisi hivyo?”
“Sisi hujifunza Biblia kwa utaratibu,” akajibu. Akiufungua mkoba wake, alitoa kile kitabu cha funzo The Harp of God akatuonyesha jinsi ya kukitumia kitabu hicho katika funzo hilo. Tulikuwa na hamu sana ya kujifunza hivi kwamba mume wangu na mimi, yule kolpota, na wanaume wengine wawili tukaambatana mara moja na mwenye duka hadi nyumbani kwake. Yule kolpota alitolea kila mmoja wetu nakala ya kitabu The Harp of God, nasi tukaanza kujifunza mara hiyohiyo. Tuliendelea na funzo letu hadi kupita sana usiku wa manane, kisha alfajiri ilipokaribia, tukaanza kujifunza nyimbo zilizoimbwa na Wanafunzi wa Biblia.
Tokea wakati huo na kuendelea, nikaanza kujifunza Biblia kwa muda wa saa kadhaa kila siku. Wanafunzi wa Biblia kutoka ng’ambo waliendelea kutupa sisi ugavi wa misaada ya kujifunza Biblia. Katika Januari 1926, nilijiweka wakfu kwa Mungu katika sala, nikiweka nadhiri ya kufanya mapenzi yake bila masharti. Baadaye katika kiangazi hicho mume wangu nami tukaonyesha wakfu wetu kwa ubatizo wa maji. Tulikuwa na tamaa yenye nguvu ya kusema na wengine kuhusu mambo tuliyokuwa tukijifunza, kwa hiyo tukaanza katika huduma ya mlango hadi mlango kwa kutumia ile trakti Message of Hope.
-