-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kupendezwa kikweli kwa Wanafunzi wa Biblia katika kusaidia watu kulidhihirishwa na jinsi walivyofanya kazi yao kikamili ambako baadaye kulikuwa zoea la kazi yao ya kuhubiri. The Watch Tower la Machi 1, 1917, lilionyesha muhtasari wa programu kama ifuatavyo: Kwanza, makolpota wangezuru nyumba katika eneo fulani, wakitoa mabuku ya Studies in the Scriptures. Kisha, wafanyakazi wachungajia wangezuru, wakifuatia majina ya wale walioandikwa na makolpota au waliokuja kwenye mikutano ya watu wote. Walijitahidi kuchochea tamaa ya kusoma fasihi, wakawatia moyo wale waliopendezwa wahudhurie hotuba zilizopangwa kipekee, na wakafanya jitihada za kupanga madarasa kwa ajili ya funzo la Biblia la Kiberoya. Ilipowezekana, makolpota wangeeneza sehemu ileile tena, na kisha wafanyakazi wa uchungaji wangefuatilia ili kuwasiliana na wale walioonyesha kupendezwa. Baadaye, wafanyakazi wengine wa darasa wangezuru nyumba zilezile wakiwa na bidhaa za kujitolea, kama vile walivyoita trakti na fasihi nyinginezo za bure walizotoa. Hilo liliwezesha kila mtu apokee angalau kitu ambacho kingechochea tamaa ya kujifunza zaidi kuhusu kusudi la Mungu.
Kolpota mmoja au wawili tu walipotumikia katika sehemu fulani, na hakukuwa kutaniko, mara nyingi makolpota walifanya kazi ya kufuatia wao wenyewe. Hivyo, wakati Hermann Herkendell na mwenzake walipoenda Bielefeld, Ujerumani, wakiwa makolpota katika 1908, waliagizwa kihususa wawajulishe watu waliopendezwa katika sehemu hiyo kwa mmoja na mwenzake na kufanyiza kutaniko. Miaka michache baadaye, The Watch Tower lilitaja makolpota wengine waliokuwa wakitoa uangalifu wa kibinafsi kwa watu waliopendezwa kufikia hatua ya kwamba walikuwa wakianzisha darasa la Wanafunzi wa Biblia katika kila mji na jiji walikotumikia.
Msaada wenye thamani kwa kazi hiyo uliandaliwa katika 1921 katika kitabu The Harp of God. Kitabu hicho kilichobuniwa hasa kunufaisha wapya kilikuwa na mwenezo wa nakala 5,819,037 katika lugha 22. Ili kusaidia wale waliopata kitabu hicho, Sosaiti ilipanga kufanya mtaala kwa njia ya barua wa funzo la Biblia kulingana na vichwa. Hilo lilitia ndani mitihani 12, iliyopelekwa katika kipindi cha majuma 12. Kwa kutumia kitabu hicho, mipango ilifanywa pia kwa ajili ya mazungumzo ya Biblia ya kikundi katika nyumba za watu waliopendezwa. Kwa kawaida idadi fulani ya Wanafunzi wa Biblia ilikuwa ikihudhuria funzo hilo.
-
-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
a Kazi ya uchungaji ilipangwa kwanza wakati wa 1915-1916 katika makutaniko 500 hivi yaliyokuwa yamemchagua Ndugu Russell kuwa pasta wao. Akiwa pasta, alikuwa amewaandikia barua akionyesha muhtasari wa kazi, ambayo hapo kwanza ilihusisha akina dada tu. Mwaka uliofuata akina ndugu pia walihusishwa katika utendaji huo. Kazi hiyo ya uchungaji, iliyofanywa na kikundi kilichochaguliwa, iliendelea hadi 1921
-