Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kuungama Dhambi Ni Takwa la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Septemba 1
    • Kumbuka maneno haya ya mwanafunzi Yakobo ambayo tayari yametajwa: “Ungameni waziwazi dhambi zenu kwa mtu na mwenzake na kusali kwa ajili ya mtu na mwenzake, ili mponywe.” Yakobo aliendelea kusema: “Dua ya mtu mwadilifu, inapofanya kazi, ina nguvu nyingi.” (Yakobo 5:16) “Mtu mwadilifu” anaweza kuwa mmoja wa “wanaume wazee wa kutaniko,” ambao Yakobo anawataja katika mstari wa 14. Katika kutaniko la Kikristo, kuna “wanaume wazee” kiroho, au wazee, waliowekwa rasmi kuwasaidia wale wanaotafuta msamaha wa Mungu. ‘Wanaume hao wazee’ hawawezi kusamehe dhambi, kwa kuwa hakuna mwanadamu ambaye amepewa mamlaka ya kumsamehe mtu ambaye amemtendea Mungu dhambi.a Hata hivyo, wanaume hao wana sifa za kiroho zinazowafanya wastahili kukaripia na kumrekebisha mtu aliyefanya dhambi nzito, wakimsaidia atambue uzito wa dhambi yake na uhitaji wa kutubu.—Wagalatia 6:1.

  • Je, Kuungama Dhambi Ni Takwa la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Septemba 1
    • Tukirejelea tena kitabu cha Yakobo, tunapata maneno haya yenye kutia moyo: “Je, kuna yeyote mgonjwa [kiroho] kati yenu? Na awaite kwake wanaume wazee wa kutaniko, nao wasali juu yake, wakimpaka mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itamponya huyo asiyejisikia vizuri, na Yehova atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.”—Yakobo 5:14, 15.

      Kwa mara nyingine tena, wanaume wazee, au wazee, wanahimizwa washughulikie mahitaji ya kondoo. Jinsi gani? Si kwa kumsikiliza tu mtu anapoungama. Badala yake, kwa kuwa ugonjwa wa kiroho unahusika, wazee wanapaswa kuchukua hatua ili ‘kumponya mtu huyo asiyejisikia vizuri.’ Kuna mambo mawili yaliyotajwa na Yakobo ambayo yanaweza kufanywa.

      Kwanza, Yakobo anataja ‘kupaka mafuta.’ Hilo linarejelea nguvu za kuponya za Neno la Mungu. Mtume Paulo alisema kwamba “neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu . . . nalo linaweza kutambua fikira na makusudio ya moyo,” kwa kuwa linapenya ndani kabisa katika akili na moyo wa mtu. (Waebrania 4:12) Kwa kutumia Biblia kwa ustadi, wanaume wazee wanaweza kumsaidia mtu aliye mgonjwa kiroho aone chanzo cha tatizo lake na kuchukua hatua zinazofaa kurekebisha mambo mbele za Mungu.

      Kisha, anataja “sala ya imani.” Ingawa sala za wanaume wazee haziwezi kumfanya Mungu asifuate haki, sala hizo ni muhimu kwa Mungu, ambaye anatamani kusamehe dhambi kwa msingi wa fidia, au dhabihu ya ukombozi ya Kristo. (1 Yohana 2:2) Mungu yuko tayari kumsaidia mtenda dhambi yeyote anayetubu kikweli na anayefanya “matendo yanayostahili toba.”—Matendo 26:20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki