-
Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Kwa sababu Mashahidi wengi walilazimika kukimbia, idadi ya makutaniko ilipungua kutoka 108 hadi 89. Sasa jiji la Brazzaville lina wahubiri 1,903 katika makutaniko 23 na Pointe-Noire lina wahubiri 1,949 katika makutaniko 24.
-
-
Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Zaidi ya miaka 50 imepita tangu Etienne Nkounkou, Augustin Bayonne, na Timothée Miemounoua walipojifunza kweli kwa kutumia kitabu ‘Kweli Itawaweka Huru.’ Katika kipindi hicho, maelfu ya watu nchini Kongo (Brazzaville) wameiga imani yao na wengine wengi wanaendelea kufanya hivyo, kukiwa na matarajio ya ongezeko kubwa zaidi wakati ujao. Zaidi ya mafunzo ya Biblia 15,000 yanaongozwa, mara tatu na nusu ya idadi ya wahubiri! Idadi ya waliohudhuria Ukumbusho iliongezeka hadi 21,987 mwaka wa 2003. Mwishoni mwa mwaka wa utumishi wa 2003, wahubiri 4,536 kutia ndani mishonari 15, walikuwa wakijitahidi kwa bidii kuwasaidia wengi kujifunza kweli itakayowaweka huru.—Yoh. 8:31, 32.
-