Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • Maisha ya Mishonari Katika Miaka ya 1960

      Katika Februari 1963, Fred Lukuc na Max Danyleyko waliwasili kutoka Haiti. Baada ya kuoa, Fred alitumikia akiwa mwangalizi wa mzunguko. Mwanzoni, alipotembelea makutaniko, ilikuwa vigumu kwake kutofautisha kila familia. Anasema hivi: “Sikuwajua wake wa wazee wala watoto wao. Bado akina ndugu walikuwa wakifuata desturi ya Afrika ya kati ya wake kuendelea kuitwa kwa majina ya baba zao hata baada ya kuolewa na watoto kuitwa majina ya watu wa ukoo au rafiki za familia.

      “Siku ya kwanza ya ziara yetu, ndugu walikuwa wenye haya na walisita kuzungumza nasi kwenye Jumba la Ufalme. Mkutano ulipoanza, tuliona jambo lisilo la kawaida. Ndugu na wavulana wakubwa waliketi upande mmoja wa jumba; watoto na akina dada waliketi upande mwingine. Upande wa akina ndugu ulikuwa umejaa mkutano ulipoanza, lakini kulikuwa na dada wachache upande wa pili. Mkutano ulipokuwa ukiendelea, dada wengine waliwasili wakiwa wamebeba Biblia na vitabu kwa ustadi sana vichwani, huku wakiambatana na watoto wao wachanga.

      “Nilisimama jukwaani kulisalimu kutaniko na kuwajulisha jina langu na la mke wangu. Baada ya kuwakaribisha kwa uchangamfu, nilitua, nikatazama upande wa wanaume, kisha nikasema: ‘Tafadhali akina ndugu, nawapa dakika kumi ili kila mmoja aketi na mke na watoto wake. Kuanzia sasa, tafadhali ketini na familia zenu kama wanavyofanya watu wa Yehova ulimwenguni pote.’ Walitii maagizo hayo kwa furaha.”

      Haikuwa rahisi kusafiri kwa magari ya umma. Leah, mke wa Ndugu Lukuc akumbuka: “Tulibeba vitanda vidogo vya kukunjwa, neti ya mbu, ndoo, vichujio vidogo vya maji, nguo, vitabu, magazeti, na sinema za Biblia. Ili kuonyesha sinema hizo, ilitubidi kubeba nyaya za umeme, balbu, kanda na hati za sinema, jenereta ndogo, na mtungi wa petroli. Tulibeba vitu hivyo vyote tuliposafiri kwa malori ya umma. Ili kuketi sehemu ya mbele pamoja na dereva, ilitulazimu kufika kwenye kituo cha malori saa nane usiku, la sivyo, tungeketi sehemu ya nyuma ya lori pamoja na wanyama, mizigo, na abiria wengine wengi huku tukichomwa na jua.

      “Pindi moja, baada ya kutembea kwa saa nyingi jua likituchoma, tulikuta chungu wamevamia nyumba ndogo ya udongo ambamo tulikaa. Walipanda ndoo ya maji, wakatengeneza daraja kwa miili yao hadi kwenye mkebe mdogo wenye siagi, na kula siagi yote. Usiku huo, tulikula mkate mkavu na dagaa mkebe mmoja. Ingawa tulikuwa tumechoka na tulijisikitikia, tulienda kulala na kuwaacha ndugu wakiimba nyimbo za Ufalme kwa sauti nyororo, wakiota moto nje. Ilipendeza na kutuliza sana kusikia nyimbo hizo tulipokuwa tukisinzia!”

      Mishonari Waaminifu na Wazee Wenyeji

      Kuanzia mwaka wa 1956 hadi 1977, zaidi ya mishonari 20 walitumikia nchini Kongo (Brazzaville). Ingawa nyakati nyingine maisha yalikuwa magumu kwao, kila mmoja wao alitimiza mengi katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme. Kwa mfano, wote waliotumikia kama waangalizi wa tawi walikuwa mishonari. Ndugu Seignobos aliporudi Ufaransa mwaka wa 1962, Larry Holmes aliwekwa kusimamia kazi ya kuhubiri. Baada ya Larry na mkewe Audrey kuacha utumishi wa mishonari mwaka wa 1965, Ndugu Lukuc akawa mwangalizi wa tawi.

  • Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • 1956: Mishonari wa kwanza kutoka Ufaransa wawasili mwezi wa Machi.

  • Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • 1977: Mashahidi wa Yehova wapigwa marufuku. Majengo ya ofisi ya tawi yatwaliwa, na mishonari wafukuzwa.

  • Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • 1997: Vita vya wenyewe kwa wenyewe vyazuka Juni 5. Mishonari wahamishwa.

  • Jamhuri Ya Kongo (Brazzaville)
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
    • 1999: Vita vingine vya wenyewe kwa wenyewe vyazuka. Mishonari wahamishwa tena.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki