-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Ndiyo,” aendelea Yohana, “mimi niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kwa Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakuwa wameabudu wala hayawani-mwitu wala mfano wake na ambao hawakuwa wamepokea alama juu ya kipaji cha uso wao na juu ya mkono wao.” (Ufunuo 20:4b, NW) Miongoni mwa wafalme hao, basi, wamo wale Wakristo wafia-imani ambao mapema zaidi, wakati wa kufunguliwa kwa kifungo cha kwanza, walimwuliza Yehova angengoja muda gani zaidi ili alipize kisasi cha damu yao. Wakati huo, walipewa joho jeupe na kuambiwa wangojee kitambo kidogo. Lakini sasa kisasi cha damu yao kimekwisha lipizwa kupitia kuteketezwa kwa Babuloni Mkubwa, na mataifa kuharibiwa na Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, na Shetani kutiwa ndani ya abiso.—Ufunuo 6:9-11; 17:16; 19:15, 16, NW.
11. (a) Sisi tuueleweje usemi “waliouawa kwa shoka”? (b) Ni kwa nini inaweza kusemwa kwamba wote 144,000 walikufa kifo cha dhabihu?
11 Je! mahakimu wa kifalme hawa wote 144,000 ‘waliuawa kwa shoka’ kimwili? Yaelekea, ni wachache wao kwa kulinganisha waliouawa hivyo kwa maana halisi. Ingawa hivyo, usemi huu bila shaka unakusudiwa kutia ndani Wakristo wapakwa-mafuta wote waliovumilia ufia-imani kwa njia moja au nyingine.b (Mathayo 10:22, 28) Kwa hakika, Shetani angependa wote wauawe kwa shoka, lakini, kwa kweli, si ndugu wote wapakwa-mafuta wa Yesu wanaokufa wakiwa wafia-imani. Wengi wao huuawa na ugonjwa au uzee. Hata hivyo, hao pia ni wa kile kikundi ambacho Yohana anaona sasa. Kifo cha wao wote, kwa maana fulani, ni cha dhabihu. (Warumi 6:3-5) Kwa kuongezea, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa sehemu ya ulimwengu. Kwa sababu hiyo, wao wote wamechukiwa na ulimwengu, maana yake, wakawa wafu katika macho yao. (Yohana 15:19; 1 Wakorintho 4:13) Hakuna hata mmoja wao aliyeabudu hayawani-mwitu au mfano wake, na walipokufa, hakuna hata mmoja wao aliyechukua alama ya hayawani. Wao wote walikufa wakiwa washindi.—1 Yohana 5:4; Ufunuo 2:7; 3:12; 12:11.
-
-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
b Shoka (Kigiriki, peʹle·kus) laonekana kuwa ndilo lililokuwa chombo cha kimapokeo cha kufisha katika Roma, ingawa kufikia siku ya Yohana upanga ulitumiwa kikawaida zaidi. (Matendo 12:2) Kwa hiyo, neno la Kigiriki lililotumiwa hapa, pe·pe·le·kis·meʹnon (“-liouawa kwa shoka”), lamaanisha tu “-liouawa.”
-