-
‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’Huduma ya Ufalme—2002 | Machi
-
-
11 Shirikiana na Wazee Kusaidia Wasiotenda: Wazee wangependa sana kuhangaikia wasiotenda kwa upendo. Wengi wao tayari wameanza kuhudhuria mikutano tena bila kuchochewa na mtu yeyote. Wametambua uhitaji wa kushirikiana kwa ukaribu na tengenezo la Yehova ili wawe na usalama wa kiroho unaoelezwa katika Zaburi 91. Baadhi yao sasa wako tayari kushiriki katika utumishi wa shambani tena. Ikiwa kuna wasiotenda ambao watahudhuria Ukumbusho mwezi huu, huenda wakakubali kujifunza Biblia. Ikitukia hivyo, wazee watafanya mipango ili mtu fulani ajifunze na wale wanaohitaji msaada. Ukiombwa usaidie, jitihada zako zitathaminiwa na wazee.—Rom. 15:1, 2.
-
-
“Zawadi Zikiwa Wanadamu” Huchunga Kundi la Mungu kwa HamuHuduma ya Ufalme—2002 | Machi
-
-
3 Kuwatia Moyo Wasiotenda: Wazee wanajitahidi sana kuwatia moyo wale wasio wa kawaida au wasiotenda, wakiwasaidia kurudia utendaji wao wa kutaniko kwa ukawaida. Ziara za wachungaji wenye upendo zimesaidia wengi wahudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na kujengwa kiroho hivi kwamba wameanza kushiriki tena katika huduma ya shambani. Jitihada zote hizo za wazee huonyesha upendo wa Yehova na uongozi wa Yesu Kristo. Aliweka kielelezo cha kuonyesha anawajali kondoo wake wowote ambao huenda wakawa wamekengeuka au kupotea.—Mt. 18:12-14; Yn. 10:16, 27-29.
-
-
“Zawadi Zikiwa Wanadamu” Huchunga Kundi la Mungu kwa HamuHuduma ya Ufalme—2002 | Machi
-
-
5 Wakristo fulani waliojiweka wakfu wameacha kushirikiana na kutaniko, na kuwa wasiotenda kiroho kwa sababu wamelemewa na magonjwa, matatizo ya kiuchumi, au misongo ya familia. Bila kuwachambua, wazee wanaweza kuwahakikishia kwa fadhili kwamba Yehova huwajali kondoo wake wote naye atawategemeza katika hali ngumu. (Zab. 55:22; 1 Pet. 5:7) Wachungaji wa kundi walio macho wanaweza kuwasaidia watambue kwamba ‘wakimkaribia Mungu, atawakaribia,’ na kuwapa faraja na pumziko.—Yak. 4:8; Zab. 23:3, 4.
-
-
“Zawadi Zikiwa Wanadamu” Huchunga Kundi la Mungu kwa HamuHuduma ya Ufalme—2002 | Machi
-
-
7 “Zawadi zikiwa wanadamu” wanajua kabisa mahitaji ya kiroho ya ndugu zao wakati huu wa mwaka—majira ya Ukumbusho. Huu ni wakati unaofaa kama nini kwa wazee kujitahidi zaidi kusaidia wote ambao wamekengeuka kufurahia tena shangwe na amani ya akili inayotokana na kushirikiana kwa uchangamfu na kutaniko! Tunafurahi tunapoona watu kama hao ambao “katika imani ni jamaa zetu” wakiwa kwenye mikutano ya kutaniko na katika huduma, wakionyesha tena imani yao katika dhabihu ya fidia.—Gal. 6:10; Luka 15:4-7; Yn. 10:11, 14.
-