-
MatangazoHuduma ya Ufalme—2008 | Aprili
-
-
Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia kitabu Mwabudu, hasa pamoja na watu ambao tayari wamejifunza kitabu Biblia Inafundisha na broshua Anataka. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Tumia broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je, Ziko Kweli?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! na broshua nyingine zinazopatikana katika lugha nyinginezo.
◼ Beji za kusanyiko la wilaya la 2008 zitatumwa pamoja na maagizo ya vichapo. Hakuna haja ya kuagiza beji hizo. Ikiwa kutaniko linahitaji beji zaidi, mnapaswa kuagiza kwa kutumia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Mnapaswa kuagiza vifuko vya plastiki vya beji kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevihitaji.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Mnaweza kuomba fomu hizo kwa kutumia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni akiba ya angalau mwaka mmoja. Kabla ya kutuma ombi la painia wa kawaida kwenye ofisi ya tawi, hakikisheni kwamba limejazwa kwa usahihi.
◼ Ofisi ya tawi inapaswa kuwa na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kuna mabadiliko yoyote ya anwani au namba za simu, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza Fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Mwandishi (S-29) na kuituma mara moja kwenye ofisi ya tawi. Fomu hiyo inapaswa pia kutia ndani mabadiliko yoyote ya namba ya simu ya eneo.
◼ Iwapo unapanga kutembelea nchi nyingine, na unataka kujua tarehe, wakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano au kusanyiko, unapaswa kuomba habari hizo kwenye ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Kuna orodha ya anwani za ofisi ya tawi katika ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni.
-
-
Pitio la Shule ya Huduma ya KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2008 | Aprili
-
-
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 28, 2008. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 3 hadi Aprili 28, 2008.
SIFA ZA USEMI
1. Kwa nini ni muhimu kutoa hotuba tukitegemea habari ambazo tumepewa, na tunaweza kufanyaje hivyo? [be uku. 234 fu. 1–uku. 235 fu. 1]
2. Kwa nini maswali ni muhimu tunapofundisha? [be uku. 236 fu. 1-5]
3. Maswali yanawezaje kuwasaidia wasikilizaji wetu wasababu juu ya habari fulani? [be uku. 237 fu. 3–uku. 238 fu. 1]
4. Tunapofundisha, kwa nini ni muhimu kutumia maswali kwa ustadi ili kutambua hisia za moyoni za wasikilizaji? (Met. 20:5; Mt. 16:13-16; Yoh. 11:26) [be uku. 238 fu. 3-5]
5. Kuna faida gani za kutumia tashbihi tunapofundisha? (Mwa. 22:17; Yer. 13:11) [be uku. 240 fu. 1-3]
HOTUBA NA. 1
6. Kitabu cha Marko kinakazia kanuni gani zenye kuongoza ambazo zitatusaidia kupata uhai chini ya Ufalme wa Mungu? [si uku. 186 fu. 32]
7. Roho takatifu inawasaidiaje watumishi wa Mungu leo? (Yoh. 14:25, 26) [be uku. 19 fu. 2-3]
8. Ni faida gani kubwa zaidi tunayopata kwa kusoma? [be uku. 21 fu. 3]
9. Kujifunza kunatia ndani nini? [be uku. 27 fu. 3–uku. 28 fu. 1]
10. Injili ya Luka inajengaje uhakika kwamba Maandiko ya Kiebrania yamepuliziwa na Mungu? [si uku. 192 fu. 30-31]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Kwa nini Yesu alimsahihisha mtu fulani aliyemwita “Mwalimu Mwema”? (Marko 10:17, 18) [w08 2/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Marko”]
12. Yesu alitumia mtini kuonyesha nini kuhusu taifa la Israeli? (Marko 11:12-14, 20, 21) [w03 5/15 uku. 26 fu. 2-3]
13. Malaika Gabrieli alimaanisha nini aliposema kwamba Maria ‘atachukua mimba katika tumbo lake la uzazi’ wakati roho takatifu itakapokuja juu yake na nguvu za Mungu kumfunika? (Luka 1:30, 31, 34, 35) [w08 3/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Luka”; it-2 uku. 56 fu. 2]
14. Je, wanafunzi wa Yesu walikuwa wakifanya “jambo lisilo halali katika siku ya Sabato”? (Luka 6:1, 2) [gt 31]
15. Tunaweza kupata somo gani kutokana na shauri la Yesu kwa Martha? (Luka 10:40-42) [w99 9/1 uku. 31]
-