-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kusudi la makusanyiko ya kimataifa ni nini? Baraza Linaloongoza hupanga makusanyiko hayo kila baada ya miaka michache katika majiji yaliyo mahali panapofaa—nyakati nyingine katika nchi ambako Mashahidi wa Yehova walikuwa wamepigwa marufuku. Makusanyiko hayo huwaimarisha akina ndugu na pia kuchochea kazi ya kuhubiri habari njema katika nchi hizo.
Makusanyiko hayo pia huwapa ndugu zetu nafasi ya pekee ya kujionea ‘kifungo cha kipekee cha muungano’ ambacho undugu wa ulimwenguni pote hufurahia. (Kol. 3:14) Inafurahisha kama nini kuona katika makusanyiko hayo upendo, amani, na umoja unaoshinda tofauti za kitaifa, kitamaduni, na lugha! Upendo wa kweli unaonyeshwa na watu kutoka maeneo mbalimbali wanapochangamana pamoja wakati wa vipindi vya mapumziko—wakila pamoja, wakipeana zawadi ndogo na anwani, wakipigwa picha, na kukumbatiana katika upendo wa kindugu. Wajumbe na wenyeji wengi huvalia nguo zao za kitamaduni.
Sehemu ya pekee katika makusanyiko ya kimataifa ni “Ripoti Kutoka Nchi Nyingine,” zilizotolewa siku zote nne za kusanyiko.
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Linapopanga makusanyiko ya kimataifa, Baraza Linaloongoza hufikiria ukubwa wa mahali ambapo kusanyiko litafanyiwa, idadi ya Mashahidi katika eneo hilo na idadi ya Mashahidi kutoka nchi nyingine watakaohudhuria, na ikiwa kuna mahali pa kulala pa kutosha kwa ajili ya wajumbe. Baada ya hapo, ndugu wanaotegemeka katika kila jiji ambapo kusanyiko litafanywa wanatafuta vibali kutoka kwa wenye mamlaka na kuwasiliana na wasimamizi wa mahali ambapo makusanyiko yatafanyiwa.
Kwa kuwa mara nyingi viwanja vikubwa vya michezo hutumiwa kwa ajili ya makusanyiko hayo, mipango na kazi nyingi itahitaji kufanywa ili kuhakikisha kwamba ni mahali penye kuheshimika kwa ajili ya ibada ya Yehova. Kwa mfano, nchini Peru, kwa sababu kulikuwa na mchezo wa kandanda kabla ya kusanyiko, akina ndugu hawangeweza kuingia kwenye uwanja huo kuusafisha na kupanga mambo hadi usiku wa kuamkia kusanyiko. Ingawa ni wajitoleaji 3,000 walioombwa kusaidia, ndugu na dada zaidi ya 7,000 walifikia kwenye uwanja huo saa 12 jioni na kufanya kazi usiku wote ili kuutayarisha.
-