-
Wakristo Wote wa Kweli Ni Waeneza-evanjeliMnara wa Mlinzi—2002 | Januari 1
-
-
15. Je, Mashahidi wa Yehova hugeuza watu imani kama wengine wafanyavyo siku hizi? Eleza.
15 Ni kosa kulazimisha watu wabadili dini. Bila shaka, Mashahidi wa Yehova hawafanyi hivyo.b Kwa hiyo, hawageuzi watu imani kama wengine wafanyavyo siku hizi. Badala yake, kama Wakristo wa karne ya kwanza, wao huhubiria kila mtu habari njema. Mtu yeyote anayekubali habari njema kwa kupenda, hutiwa moyo atwae ujuzi zaidi kwa kujifunza Biblia. Watu hao wenye kupendezwa hujifunza kuwa na imani inayotegemea kabisa ujuzi sahihi wa Biblia kuhusu Mungu na makusudi yake. Hivyo, wanaliitia jina la Mungu, Yehova, ili kupata wokovu. (Waroma 10:13, 14, 17) Ni juu yao kuamua kama watakubali au watakataa habari njema. Hawalazimishwi. Kama watu wangelazimishwa, kugeuza watu imani hakungekuwa na maana yoyote. Ili mtu akubaliwe na Mungu, lazima ibada yake itoke moyoni.—Kumbukumbu la Torati 6:4, 5; 10:12.
-
-
Wakristo Wote wa Kweli Ni Waeneza-evanjeliMnara wa Mlinzi—2002 | Januari 1
-
-
b Kwenye mkutano wa Tume ya Kimataifa ya Uhuru wa Kidini uliofanywa Marekani Novemba 16, 2000, mshiriki mmoja alitaja tofauti iliyopo kati ya watu wanaojaribu kulazimisha wengine wabadili imani yao na kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova. Ilisemekana kwamba Mashahidi wa Yehova wanapowahubiria watu, wanafanya hivyo kwa njia ambayo mtu anaweza kusema “Mimi sipendezwi” na afunge mlango.
-