-
Rwanda2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
SALA YA MSICHANA MDOGO YAWAOKOA
Siku moja baada ya ndege iliyowaua marais wa Rwanda na Burundi kuanguka, askari sita wa serikali walienda kwa Ndugu Rwakabubu. Macho yao yalikuwa mekundu sana, walinuka pombe, na walijiendesha kwa njia iliyoonyesha kwamba walikuwa wametumia dawa za kulevya. Wakaamuru wapewe silaha. Ndugu Rwakabubu akawaambia kwamba yeye na familia yake ni Mashahidi wa Yehova na hivyo hawana silaha.
Askari hao walijua kwamba kwa sababu Mashahidi wa Yehova hawaungi mkono upande wowote, walikataa kuunga mkono serikali, na hawakuwasaidia wanajeshi kifedha. Hilo liliwakasirisha. Gaspard na Melanie Rwakabubu, si Watutsi, lakini wapiganaji wa Interahamwe waliwaua pia Wahutu ambao hawakuwa na msimamo mkali, hasa ikiwa walidhaniwa kuwa wanawahurumia Watutsi au jeshi lililopinga serikali.
Askari hao waliwapiga Gaspard na Melanie kwa vijiti na kuwapeleka pamoja na watoto wao watano katika chumba cha kulala. Wakaondoa mashuka kitandani na kuanza kuwafunika nayo. Baadhi yao walikuwa na makombora mikononi, hivyo ilikuwa wazi walitaka kuwaua. Gaspard akawauliza, “Tunaweza kusali tafadhali?”
Kwa dharau, askari mmoja alikataa ombi lao. Kisha, baada ya mazungumzo fulani askari hao wakakubali, lakini shingo upande. Wakawaambia “Sawa, tunawapa dakika mbili msali.”
Wakasali kimya-kimya, lakini Deborah Rwakabubu, aliyekuwa na umri wa miaka sita, akasali kwa sauti: “Yehova, watu hawa wanataka kutuua, lakini tutawarudiaje watu niliowahubiria na kuwaachia magazeti matano nikiwa na Baba? Wanasubiri tuwarudie na wanahitaji kujua kweli. Nakuahidi kwamba tusipouawa, nitakuwa mhubiri, nibatizwe, na kuwa painia! Yehova, tuokoe!”
Waliposikia sala hiyo, askari hao wakashangaa. Mwishowe, mmoja wao akasema: “Kwa sababu ya sala ya huyu msichana mdogo, hatutawaua. Wengine wakija, waambie kwamba tayari tumekuwa hapa.”b
-
-
Rwanda2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
b Deborah alifanya maendeleo na kuwa mhubiri, akabatizwa akiwa na umri wa miaka kumi, na sasa yeye ni painia wa kawaida pamoja na mama yake.
-