-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Baada ya muda, Baraza Linaloongoza lilitoa kibali cha kutafsiri Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kufikia wakati huo, akina ndugu walikuwa wakitumia Biblia iliyotafsiriwa miaka 150 kabla ya hapo, yenye lugha iliyopitwa na wakati na yenye maneno mengi magumu. Kikundi cha watafsiri wa lugha ya Kikroatia kiliongoza katika kazi hiyo, na kilishirikiana kwa ukaribu na vikundi vya watafsiri wa Kiserbia na Kimakedonia. Wote walifaidika kutokana na ushirikiano huo na kazi ya kila mmoja.
Ijumaa, Julai 23, 1999, ni siku itakayokumbukwa kwa muda mrefu na Mashahidi wa Yehova huko Kroatia, vilevile Bosnia na Herzegovina, Montenegro, Serbia, na Makedonia. Kwenye Makusanyiko yote manne ya Wilaya ya “Neno la Mungu la Kiunabii,” Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika Kikroatia na Kiserbia, na wahudhuriaji wakaambiwa kwamba kazi ya kutafsiri Biblia ya Kimakedonia inaendelea vizuri. Wahudhuriaji walipiga makofi kwa dakika kadhaa na ikawabidi wasemaji wanyamaze kimya. Wahudhuriaji walishangilia sana, na wengi wao hawangeweza kuzuia machozi yao ya furaha. Mzee mmoja wa kutaniko ambaye ametumika kwa muda mrefu alisema: “Siamini kwamba nimeiona siku hii!”
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Biblia yote nzima ilitolewa katika mwaka wa 2006 katika lugha hizo tatu.
-