-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Henrik Kovačić, ambaye ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi huko Kroatia, anakumbuka: “Kwa karibu mwaka mmoja, nilitumika pamoja na mke wangu nikiwa mwangalizi wa mzunguko mwishoni mwa juma, na baadaye nikawa mwangalizi anayesafiri wa wakati wote. Ndugu walikuwa maskini sana, na mara nyingi tulikaa mahali ambapo hapakuwa na mabomba ya maji wala vyoo vinavyotumia maji. Lakini ndugu walithamini sana ziara zetu na walituonyesha upendo na ukarimu wa pekee sana. Mara nyingi, walituachia vitanda vyao na walitupa chakula, ingawa wao wenyewe walikuwa na mapato kidogo sana. Katika makutaniko fulani, ili tusiwe mzigo kwao, tulikaa katika nyumba tofauti kila usiku.”
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
“Je, Watu Wanaruhusiwa Kuzungumza Kuhusu Mchezo wa Kandanda?”
HENRIK KOVAČIĆ
ALIZALIWA 1944
ALIBATIZWA 1962
MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Alitumika mwaka wa 1973 akiwa mwangalizi anayesafiri mwishoni mwa juma, na baadaye kuanzia mwaka wa 1974 mpaka 1976, aliwekwa rasmi kuwa mwangalizi anayesafiri wa wakati wote. kwa sasa yeye ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kroatia.
HATUKUJUA kamwe ikiwa tungeweza kurudi nyumbani kutoka katika huduma. Mara nyingi, polisi walitukamata na kutuhoji. Kwa kawaida, watu walikuwa na maoni yasiyofaa kuhusu kazi yetu.
Pindi moja kwenye kituo cha polisi, niliambiwa kwamba tuliruhusiwa tu kuzungumza kuhusu Mungu mahali fulani palipochaguliwa kwa ajili ya kusudi hilo na si barabarani wala nyumba kwa nyumba. Kama Nehemia, nilitoa sala fupi ili kumwomba Yehova anisaidie kupata maneno yanayofaa. Kisha, nikamuuliza mchunguzi huyo, “Je, watu wanaruhusiwa kuzungumza kuhusu mchezo wa kandanda wakiwa uwanjani tu au wanaweza kufanya hivyo mahali pengine pia?” Alijibu kwamba watu wanaweza kufanya hivyo mahali popote pale. Nikamwambia hivi: “Hivyo, basi, unaweza pia kuzungumza kuhusu Mungu mahali popote pale, si kanisani tu au mahali fulani pa ibada.” Ingawa tulihojiwa kwa muda wa saa tano, mimi na mwenzangu tuliachiliwa huru.
Mimi na mke wangu, Ana, tunapokumbuka miaka 40 ya utumishi, tunaweza kusema kwamba hatuwezi kuacha utumishi huo kwa ajili ya kitu kingine chochote ulimwenguni. Mimi na mke wangu tumepata pendeleo la kuwasaidia watu 70 hivi kujifunza kweli. Kila mgawo ambao Yehova anataka tufanye unaboresha tu maisha yetu.
-