Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Punde si punde, ndugu walipata jengo la kiwanda katikati ya mji wa Zagreb, Kroatia. Waliligeuza jengo hilo kuwa Jumba la Ufalme maridadi lenye viti 160 hivi na wakaongeza ofisi ndogo ya kuchapishia vichapo. Jumba hilo la Ufalme lilitumiwa pia kwa ajili ya makusanyiko na lilianza kutumiwa mwaka wa 1957 wakati kusanyiko la kwanza la wilaya lilipofanywa kwa ajili ya Mashahidi kutoka sehemu zote za Yugoslavia. Miaka michache baadaye, ndugu walinunua nyumba moja katikati ya mji wa Zagreb kwenye Barabara ya Kamaufova, ambayo ilitumiwa na familia ya Betheli mpaka mwaka wa 1998.

  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • MIPANGO BORA INACHOCHEA UKUZI WA KIROHO

      Katika mwaka wa 1960, waangalizi wanaosafiri walipewa migawo ya kuyasaidia na kuyatia moyo makutaniko. Ndugu wengine waliombwa watumike wakiwa waangalizi wa mizunguko wa “miisho-juma.” Ndugu hao walikubali kutumia siku zao za likizo ili kusafiri na kuwatia moyo akina ndugu na kuwasaidia kuwa na umoja katika siku hizo za mapema.

      Henrik Kovačić, ambaye ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi huko Kroatia, anakumbuka: “Kwa karibu mwaka mmoja, nilitumika pamoja na mke wangu nikiwa mwangalizi wa mzunguko mwishoni mwa juma, na baadaye nikawa mwangalizi anayesafiri wa wakati wote. Ndugu walikuwa maskini sana, na mara nyingi tulikaa mahali ambapo hapakuwa na mabomba ya maji wala vyoo vinavyotumia maji. Lakini ndugu walithamini sana ziara zetu na walituonyesha upendo na ukarimu wa pekee sana. Mara nyingi, walituachia vitanda vyao na walitupa chakula, ingawa wao wenyewe walikuwa na mapato kidogo sana. Katika makutaniko fulani, ili tusiwe mzigo kwao, tulikaa katika nyumba tofauti kila usiku.”

  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 179]

      “Je, Watu Wanaruhusiwa Kuzungumza Kuhusu Mchezo wa Kandanda?”

      HENRIK KOVAČIĆ

      ALIZALIWA 1944

      ALIBATIZWA 1962

      MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Alitumika mwaka wa 1973 akiwa mwangalizi anayesafiri mwishoni mwa juma, na baadaye kuanzia mwaka wa 1974 mpaka 1976, aliwekwa rasmi kuwa mwangalizi anayesafiri wa wakati wote. kwa sasa yeye ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kroatia.

      HATUKUJUA kamwe ikiwa tungeweza kurudi nyumbani kutoka katika huduma. Mara nyingi, polisi walitukamata na kutuhoji. Kwa kawaida, watu walikuwa na maoni yasiyofaa kuhusu kazi yetu.

      Pindi moja kwenye kituo cha polisi, niliambiwa kwamba tuliruhusiwa tu kuzungumza kuhusu Mungu mahali fulani palipochaguliwa kwa ajili ya kusudi hilo na si barabarani wala nyumba kwa nyumba. Kama Nehemia, nilitoa sala fupi ili kumwomba Yehova anisaidie kupata maneno yanayofaa. Kisha, nikamuuliza mchunguzi huyo, “Je, watu wanaruhusiwa kuzungumza kuhusu mchezo wa kandanda wakiwa uwanjani tu au wanaweza kufanya hivyo mahali pengine pia?” Alijibu kwamba watu wanaweza kufanya hivyo mahali popote pale. Nikamwambia hivi: “Hivyo, basi, unaweza pia kuzungumza kuhusu Mungu mahali popote pale, si kanisani tu au mahali fulani pa ibada.” Ingawa tulihojiwa kwa muda wa saa tano, mimi na mwenzangu tuliachiliwa huru.

      Mimi na mke wangu, Ana, tunapokumbuka miaka 40 ya utumishi, tunaweza kusema kwamba hatuwezi kuacha utumishi huo kwa ajili ya kitu kingine chochote ulimwenguni. Mimi na mke wangu tumepata pendeleo la kuwasaidia watu 70 hivi kujifunza kweli. Kila mgawo ambao Yehova anataka tufanye unaboresha tu maisha yetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki